Na  Bashir  Yakub.

Tumekuwa  tukisikia   fulani  amepatikana  na  hatia  ya  kuua  bila  kukusudia  au  fulani  ameua  bila  kukusudia,  je  unajua  nini  maana  ya  kuua  bila  kukusudia  kisheria. Mara  ya mwisho  neno  kuua  bila  kukusudia  limesemwa sana baada ya  hukumu katika kesi  iliyohusu kifo cha mwanahabari  Daudi  Mwangosi.  Yapo  mengi  ya  kujua  kuhusu  kuua  bila  kukusudia.

Kifungu  cha  195, sura ya 16, Kanuni  za  adhabu ndicho  huzungumzia  kuua  bila  kukusudia.

1.NINI MAANA YA KUUA BILA KUKUSUDIA.

Katika  sheria  kuua  bila  kukusudia  (manslaughter)  kunatofautishwa  na  kuua  kwa  kukusudia(murder). Kuua  bila  kukusudia  ni  kuua ambako  muuaji   anatenda  kitendo  kinachopelekea  kifo  lakini hakuwa na  nia,dhamira au  lengo  la  kusababisha mtu afe. 

Wakati  kuua  kwa  kukusudia  ni  pale  mtu  anapotenda  tendo   ambalo  linapelekea  mauaji  ya  mtu   lakini  amefanya  hivyo  akiwa  amedhamiria   kuua.  Kwahiyo  haraka  utaona  kuwa  tofauti  kubwa  ya  kuua kwa  kukusudia  na  ile  ya  kuua  bila  kukusudia  ni  dhamira, nia au  lengo. 

Dhamira,nia au lengo  likiwa ni kuua,  basi huko  ndiko  kuua  kwa  kukusudia. Na dhamira,nia au lengo  likiwa sio kuua lakini  bahati  mbaya  mtu  akafa  basi  hiyo  itakuwa  ndio  kuua bila kukusudia. Tutajuaje  huyu  aliua  kwa  kukusudia  na  huyu  hakukusudia,  tutaona  hapa  chini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...