Karibuni sana katika mkutano wetu muhimu tunaofanya leo tukiwa hapa Dodoma mara baada ya kumalizika kwa kikao cha juu cha Jumuiya yetu yaani Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM Taifa.
Tarehe 10 Agost mwaka huu kilianza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM Taifa kikafuatia kikao cha Kamati ya Maadili, kufuatia kikao cha Kamati ya Utekelezaji ya Baraza Kuu la UVCCM Taifa na baadaye Baraza Kuu la UVCCM Taifa. Jumla ya Agenda tisa (9) zilijadiliwa.
Baraza Kuu limeridhika na taarifa kadhaa kuhusiana na agenda mbali mbali na kupokea taarifa moja nyeti na muhimu kwa Jumuiya. “Ripoti ya uchunguzi wa Shamba la UVCCM Na. 454 MBYLR lenye ekari 210” lililopo Igumbilo Wilaya ya Iringa mjini Mkoani Iringa ambalo limeuzwa kwa Ndugu Suhail Ismail Thakore kinyume na taratpia pia viwanja hivyo kuuzwa kwa watu mbali mbali na kuwahusisha Viongozi kadhaa wenye dhamana ndani ya Jumuiya yetu.
Baada ya kupata taarifa za uuzaji wa shamba hilo Mali ya UVCCM, kwa Mamlaka iliyonayo Kamati ya Utekelezaji Taifa Ibara 91 (d), ilimwachia Mamlaka Mwenyekiti wa UVCCM Taifa kuunda na kuteua wajumbe watatu wa Kamati ya Utekelezaji ya Baraza Kuu la UVCCM Taifa kuenda kufanya uchunguzi wa kadhia hiyo.
Nichukue nafasi hii kuishukuru kwa dhati
Kamati ya uchunguzi iliyoongozwa na;
Kamati ya uchunguzi iliyoongozwa na;
Ndugu Mariam Chaurembo - Mwenyekiti
Ndg Juma Homela - Katibu
Ndg AmirMkalipa Mjumbe
Ndugu Ally Nassor Mjumbe
Kwa kufanikisha kazi waliyopewa na Jumuiya na hatimaye kuwasilisha ripoti yao ambayo ilibaini mambo kadhaa machafu kinyume na miongozo ya Chama na Jumuiya yetu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...