Katibu
Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii,Meja Jenerali Gaudence Milanzi
akipokea salamu ya utii kutoka kwa askari wa Shirika la Hifadhi za Taifa
(TANAPA) na Maafisa wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (hawapo
pichani) wakati wa ufungaji mafunzo kwa askari na maafisa hao
yaliyofanyika katika kambi ya mafunzo ya Mlele mkoani Katavi
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Meja Jenerali Gaudence Milanzi
akikagua gwaride wakati wa kufunga mafunzo kwa askari wa Shirika la
Hifadhi za Taifa (TANAPA) na Maafisa wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro
yaliyofanyika katika kambi ya mafunzo ya Mlele mkoani Katavi.
Askari na Maafisa wa Hifadhi za Taifa wakionesha umahiri katika
matumizi ya silaha wakati wakionesha kwa vitendo mafunzo ya kijeshi
waliyopata katika kambi ya Mlele mkoani Katavi ikiwa ni sehemu ya
kubadili utendaji kazi wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na
Utalii kuendeshwa katika mfumo wa jeshi usu.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Meja Jenerali Gaudence Milanzi
akitizama matundu ya risasi zilizolengwa na mmoja wa askari wa uhifadhi
waliohitimu mafunzo ya kijeshi katika kambi ya Mlele mkoani Katavi.Kulia
kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan
Kijazi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...