Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye( kushoto) akiangalia bidhaa za filamu na muziki zilizokamatwa katika zoezi la kushtukiza la ukamataji wa bidhaa hizo katika soko la Kariakoo jijini Dar es Salaam zilizoingizwa nchini kinyume na sheria, kulia ni Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bi. Joyce Fissoo.
Mitambo ya kuzalishia bidhaa za filamu na muziki kama zilivyokutwa katika kampuni ya Aguster kariakoo jijini Dar es Salaam katika zoezi la kushtukiza la ukamataji wa bidhaa hizo zilizoingizwa sokoni kinyume na sheria na hivyo kuikosesha serikali mapato kupitia kodi. Picha zote na Lorietha Laurence WHUSM.

Na Raymond Mushumbusi WHUSM

Kilio cha wizi wa kazi za sanaa nchini kimekuwa cha siku nyingi hali inayosababisha wasanii wengi kukosoa haki ya kazi zao kwani baadhi ya watu wamekuwa wakitumia kazi zao kujinufaisha wenyewe na wasanii kubaki wakiwa hawana maendeleo yoyote kutokana na kazi zao ukilinganisha na wasanii wa nchi jirani za Afrika ya Mashariki na duniani kwa ujumla.

Ikumbukwe katika halfa iliyoandaliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli kwa kuwashukuru makundi ya watu mbalimbali wakiwemo wana habari, wasanii na wanamichezo kwa ujumla Mhe. DKt Magufuli aliagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kusimamia kazi za wasanii na kuhakikisha wanakamata kazi zote ambazo hazina stika ya TRA.

Katika kutekeleza agizo hilo hivi karibuni Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye alifanya zoezi la kushtukiza la kukagua kazi za wasanii ambazo hazina stika ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ambazo zinakwepa kulipa kodi katika soko la Kariakoo Jijini Dar es Salaam na kuahidi  kwamba zoezi hilo litafanyika nchi nzima.
Katika zoezi hilo Serikali ilifanikwa kukamata jumla ya  bidhaa za filamu na muziki 111,802 ambapo 111,529 ni za wasanii wa nje zilizoingia nchini kinyume na sheria huku bidhaa 273 za wasanii wa ndani zikiwa hazina stika ya ushuru wa bidhaa kutoka Mamlaka ya  Mapato Tanzania(TRA).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...