Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ambaye ni Mbunge wa Namtumbo
Mhandisi Edwin Ngonyani anawatarifu wakazi wa Namtumbo na watanzania kwa
ujumla kuwa habari iliyochapishwa kwenye gazeti la Mseto si ya kweli na ina lengo la
kumchafua katika utendaji wake wa kazi.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mhandisi Ngonyani amesikitishwa na taarifa hiyo
iliyochapishwa kwenye gazeti la Mseto la tarehe 4 Agosti 2016 ikiwa kwenye ukurasa
wa kwanza yenye kichwa cha habari kilichoandikwa "WAZIRI AMCHAFUA JPM".
Habari hiyo ikiwa na nukuu "Waziri wa Serikali ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kudaiwa kupokea fedha za kufanyia kampeni za
ubunge kutoka kwa wawekezaji wa nje kwa kuwahidi kuwa mitaji yao nchini itakuwa
salama".
Aidha Mhandisi Ngonyani amesisitiza umuhimu wa waandishi wa habari kuandika
habari zenye taarifa kamili na kweli ili kuepuka upotoshwaji.
Habari hiyo ilikuwa imedai kuwa Mbunge huyo ambaye ni Naibu Waziri wa Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano amepokea kiasi cha dolla elfu 65 kwa Bw. James Sinclair ili
zimsaidie kupata nafasi ya ubunge.
Imeongeza kuwa alipewa kiasi cha dolla elfu 25 kutoka kwa Dr. Alphonce Koigi Machari
ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Trans Century ili apate nafasi hiyo hiyo ya
ubunge.
Mhandisi Ngonyani amelitaka gazeti hilo kukanusha taarifa hiyo kwa haraka
iwezekanavyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...