WAZIRI wa Habari,Utamaduni, Michezo na Sanaa, Nape Nnauye amesema kuwa uoneshaji mbashara wa mashindano ya ligi kuu Barani Ulaya 
yanayoanza kutimua vumbi leo na kuonyeshwa mbashara na TV 1 ni fursa kwa wachezaji wa ndani kujifunza mbinu mbalimbali katika kuboresha ligi za ndani.
Nape amyesema hayo jana wakati wa uzinduzi wa uoneshaji wa mbashara wa TV 1 wa mashindano ya Ligi kuu Barani Ulaya yanayoanza kutimua vumbi leo amesema kuwa TV 1 kuonesha mashinadano hayo yanaongeza fursa kwa wizara yake katika wananchi kuweza kupata habari za michezo.

Amesema kuwa ni fursa ya kwa watu kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo ndani kupitia oneshaji huo kutokana na watu wa nje wanaamini Mlima Kilimanjaro uko Kenya na wakitaka kufika lazima wafanye hivyo wakati haiko hivyo.
Amesema kuwa sekta ya Wizara yake ni kubwa hivyo wananchi wanafursa ya kufanya matangazo mbalimbali katika mashindano hayo ya ligi kuu barani Ulaya.
Nape amesema kuwa hata yeye ni shabiki wa timu wa Manchester United na anatabiri kuwa wataingia fainali katika mshindano hayo na kuweza kuibuka kuwa mabingwa barani ulaya.
Aidha amesema sekta ya utalii wanatakiwa kutumia fursa ya mashindano ya kuhamasisha utalii ikiwa ni pamoja na kuelezea mlima kiliimanjaro uko Tanzania na Sio Nchini Kenya na watalii wakisafiri wafike Tanzania kwa kufanya hivyo watakuwa wameisadia serikali kupata mapato ya moja kwa moja.
Aidha ametaka kuanza kwa mashindano hayo kuongeza ujuzi wa wachezaji katika kuweza kubadili soka la ndani kuwa na ushindani wenye tija wa kusonga mbele katika mchezo wa miguu.

Waziri wa Habari,Utamaduni, Michezo na Sanaa, Nape Nnauye akizungumza jana katika uzinduzi wa uoneshaji mbashara wa mashindano ya ligi kuu Barani uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari,Utamaduni, Michezo na Sanaa, Nape Nnauye akipokea zawadi ya king'amuzi kutoka kwa Mwenyekiti wa bodi wa TV 1,Balozi Paul Rupia katika uzinduzi wa uoneshaji mbashara wa mashindano ya ligi kuu Barani uliofanyika jijini Dar es Salaam. 
Waziri wa Habari,Utamaduni, Michezo na Sanaa, Nape Nnauye akiteta jambo na Mkurugenzi wa TV I,Joseph Sai katika uzinduzi uoneshaji mbashara wa mashindano ya ligi kuu Barani uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...