Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa, Mhe. Jean-Marc Ayrault (watatu
kulia) na ugeni wake wakisikiliza maelezo kuhusu Bandari ya Dar es Salaam
kutoka kwa Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Dk.
Leornard Chamuriho (kushoto). Kulia ni Kaimu Meneja Bandari ya Dar es
Salaam, Bw. Habel Mhanga.
Baadhi ya Maafisa kutoka nchini Ufaransa ambao waliongozana na Waziri wa
Mambo ya Nje wa nchi hiyo kutembelea Bandari ya Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Dk. Leornard
Chamuriho (kushoto) akifafanua jambo kwa mmoja wa waandishi wa habari
kutoka nchini Ufaransa wakati wa ziara ya Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi
hiyo katika Bandari ya Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA),
Mhandisi Deusdedit Kakoko (kulia) akifurahia jambo na Katibu Mkuu wa
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Dk. Leornard Chamuriho (wapili
kulia) na baadhi ya Maafisa wa Serikali waliofanikisha ziara ya Waziri wa
Mambo ya Nje wa Ufaransa kutembelea Bandari ya Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...