Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa, Mhe. Jean-Marc Ayrault (watatu kulia) na ugeni wake wakisikiliza maelezo kuhusu Bandari ya Dar es Salaam kutoka kwa Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Dk. Leornard Chamuriho (kushoto). Kulia ni Kaimu Meneja Bandari ya Dar es Salaam, Bw. Habel Mhanga.
Baadhi ya Maafisa kutoka nchini Ufaransa ambao waliongozana na Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo kutembelea Bandari ya Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Dk. Leornard Chamuriho (kushoto) akifafanua jambo kwa mmoja wa waandishi wa habari kutoka nchini Ufaransa wakati wa ziara ya Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo katika Bandari ya Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Deusdedit Kakoko (kulia) akifurahia jambo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Dk. Leornard Chamuriho (wapili kulia) na baadhi ya Maafisa wa Serikali waliofanikisha ziara ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa kutembelea Bandari ya Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...