Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Mhongo akizungumza na wadau mbalimbali wa uchimabji wa madini ya Jasi (Gypsum) na Makaa ya mawe nchini leo Jijini Dar es salaam na kuwaagiza wawakilishi
wa wachimbaji wa madini ya Jasi (Gypsum) kutoka kanda zote hapa nchini kufikia Agosti 10-11 kupeleka orodha
kamili ya majina ya wachimbaji wadogo wadogo wa madini ya Jasi (Gypsum) na makaa ya mawe katika wizara ya Nishati na madini.
Hayo ameyasema wakati akizungumza na wadau mbalimbali wa uchimbaji wa madini jijini Dar es Salaam leo amesema kuwa orodha ya majina wachimbaji wa madini ikipelekwa watafanya marekebisho ili kuweza kukabiliana na changamoto zinazowakabili.
Mhandisi wa madini ya Jasi(Gypsum) kutoka kanda ya kusini Benjamin Mchwapaka akielezea changamoto zinazopatikana ukanda wao wa Kusini ambazo zinawafanya kufikia maleno yao ya kusambaza madini hayo kwenye viwanda tofauti hapa nchini.
amesema kuwa mpaka sasa kuna leseni 1,115 zilizosajiliwa na maeneo yanayopatikana ni Kilwa Makaganga, Hoteli Tatu na Nondwa ambapo kuanzia 2009 uchimbaji umeongezeka na kuongeza upatikanaji wa jasi. Katika leseni hizo 7 ni za uchimbaji mkubwa , 22 ni za utafutaji wa ligi huku 1086 zikiwa ni za wachimbaji wadogo na kati ya hizo 306 uchimbaji unafanyika.
Changamoto kubwa inayosababisha kushindwa kufikia maleni hayo ni pamoja na vifaa ikiwemo na ukosefu wa mitaji kwa wachimbaji hao huku wakiwa na mikataba isiyokuwa na tija kutoka kwa viwanda vinayochukua madini hayo kwani wanapatiwa miakatab ya siku 28 na malipo yanachelewa kufikia miezi 2 hadi 4. Ukiachilia hilo pia miundo mbinu imekuwa shida hasa kipindi cha masika wanshindwa kuchimba, ukosefu wa taarifa za kutosha pia kina kirefu cha madini hayo ikiwemo na tozo zinazokera.
Mjiolojia na Mkuu wa Kitengo cha Kanzi Data (Database) Nchini,Masota Magigita akitolea ufafanuzi kuhusiana na masuala ya upatikanaji wa madini ya Makaa ya mawe mbele ya Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Mhongo leo Jijini Dar es salaam.
Baadhi ya wadau mbalimbali wa uchimbaji madini hapa nchini wakimsikiliza waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Mhongo jijini Dar es Salaam leo. Picha na Yasri Adam, Globu ya Jamii.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...