Waziri  wa Nchi - Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Bumbuli, January Makamba akielezea hali ya upatikanaji wa umeme katika jimbo lake, mara Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhogo alipofanya ziara katika jimbo lake. Profesa Muhongo yupo mkoani Tanga kwa ajili  ya kukagua miradi ya  umeme  vijijini inayotekelezwa na Wakala wa Nishati  Vijijini (REA) pamoja na kuzungumza na wananchi.

 Mbunge wa Lushoto, Shaban Shekilindi akielezea utekelezaji wa miradi ya usambazji wa umeme vijijini inayotekelezwa na REA katika jimbo lake mbele ya Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo na wakazi wa jimbo hilo (hawapo pichani)
 Sehemu ya wakazi wa eneo la Mlola wilayani Lushoto mkoani Tanga wakifuatilia hotuba iliyokuwa inatolewa na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo
 
 Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Tanga, Mhandisi Zephania Maduhu (katikati) akielezea mikakati ya ofisi yake katika kuimarisha  shughuli za uchimbaji madini katika mkoa huo. Kulia ni Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na kushoto ni Mbunge wa Lushoto, Shaban Shekilindi.
 Kiongozi wa Kikundi cha Wazee wa Utamaduni cha Mlola,  Khalfan Bakari (kushoto) akitoa maoni yake mbele  ya  Waziri wa Nishati na Madini,Profesa Sospeter Muhongo (kulia)
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akipanda mti wa kumbukumbu katika eneo la Lukozi wilayani Lushoto mkoani Tanga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...