Balozi wa Tamasha la Majimaji Selebuka, Nathan Mpangala (katikati), akielezea jambo kuhusu tukio la kesho ambalo atalitumia kukutana na baadhi ya wakaazi wa Dar es Salaam, kuanzia saa 11 jioni katika viwanja vya “Nafasi Art Space, Mikocheni, jijini Dar es Salaam, ambapo atatumia nafasi hiyo kusimulia yaliyojitokeza katika tamasha hilo lililofanyika Songea miezi michache iliyopita. Wengine katika picha ni wadau wa tamasha hilo, Grace Matovolwa na Mussa Sango.
Mdau wa Tamasha la Majimaji Selebuka, Mussa Sango akisisitiza umuhimu wa wakaazi wa Dar es Salaam kushiriki mazungumzo hayo yatakayofanyika kesho kuanzia saa 11 jioni katika viwanja nya Nafasi Art Space, Mikocheni, jijini Dar es Salaam. Ni tukio la wazi, halina kiingilio.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...