Mkuu wa wilaya ya Handeni Mh. Gdwin GOndwe akisalimiana na mkazi wa kijiji cha nyasa.
Mkuu
waa Wilaya ya Handeni,Mh Godwin Gondwe Jana alifanikiwa kusuluhisha
mgogoro wa mpaka uliokuwa ukivihusisha vijiji viwili vya kata ya
kang'ata wilayani Handeni .Vijiji hivyo ni Madebe na Nyasa ambao walikua
hawafahamu mpaka wao unaishia wapi,suluhu hiyo ilifanikiwa kumalizwa na
mkuu wa wilaya na mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya
Handeni ,Bwa.William Makufwe.
DC
Gondwe pia aliwataka wananchi na viongozi wajikite katika shughuli za
kimaendeleo badala ya kujikita kwenye suala la mipaka ,Kwa madai wapate
maeneo ya kulima wakati wakigombania maeneo ili wauze. Amewaonya
wasiuze ardhi kiholela na kufanya vizazi vijavyo kuwa watumwa kwenye
ardhi yao.
Mkuu
wa wilaya Mh.Godwin Gondwe akimsikiliza Mkurugenzi mtendaji wa wilaya
ya Handeni,Ndugu William Makufwe (pichani kushoto) akitoa ufafanuzi kwa
wananchi wa vijiji vya nyasa na madebe.
Mwenyekiti
wa kijiji cha nyasa na madebe wakipeana pongezi baada ya kujua mipaka
yao huku wakisistizwa kujikita zaidi katika masuala ya maendeleo.
Mkuu
wa wilaya ya Handeni Mh. Gondwe akipeana mkono wa pongezi na Mwenyekiti
wa kijiji cha Nyasa baada ya kupata mpaka wa maeneo yao.
Mkuu
wa wilaya ya handeni Mh.Gondwe akizungumza na wananchi wa vijiji vya
nyasa na madebe akiwakataza wasiuze ardhi kiholela na wasigombanie
maeneo ili wayauze.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...