Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mohamed Chande Othman , akionesha   nakala ya kitabu cha Mpango Mkakati wa miaka mitano (5) wa Mahakama ya Tanzania, alipokuwa katika Mkutano kati yake na Waandishi wa Habari uliofanyika mapema leo katika Ofisi za Mahakama ya Rufani (T), lengo la Mkutano huo lilikuwa ni kutoa taarifa juu ya uzinduzi rasmi wa Mpango huo utakaofanywa na Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Kassim M. Majaliwa kwa niaba ya Mhe. Rais, mnamo tarehe 21.09.2016, katika jengo jipya la Mahakama ya Wilaya ya Kibaha mkoani Pwani. Kushoto ni Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Ferdinand Wambali, kulia ni Mhe. Katarina Revocati, Msajili Mkuu, Mahakama ya Tanzania.
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mohamed Chande Othman akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari walioshiriki katika Mkutano huo, miongoni mwa mambo aliongelea ni pamoja na uzinduzi rasmi wa Mradi wa Maboresho wa huduma utakaotekelezwa kwa kushirikiana na Benki ya Dunia (WB).
 Baadhi ya Waandishi wa Habari wakiwa kazini. 
(Picha na Mahakama ya Tanzania)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...