Na Abel Daud wa Globu ya Jamii, Kigoma
Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako amewahakikishia wanafunzi kote nchini kwamba Serikali ya awamu ya tano imejipanga kuhakikisha inatengeneza mazingira rafiki ili kila atakayefaulu aweze kuendelea na hatua ya juu zaidi ya kielimu.
Hayo ameyasema leo hii Wilayani Kasulu alipotembelea Shule ya Msingi Mwenge pamoja na Chuo cha Elimu ya Taifa Kasulu kukagua miundombinu tayari kwa kupokea wanafunzi wa diploma kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma maarufu kama UDOM.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Kanali Martin Mkisi amemueleza Waziri Ndalichako kuwa Wilaya yake imejipanga kuinua elimu kwa kiwango kikubwa na kuwataka watumishi wa halmashauri za Kasulu pamoja na wananchi kwa ujumla kumpa ushirikiano ili kufikia malengo waliyojipangia ya kuinua elimu wilayani hapo.
Prof.Ndalichako ameupongeza uongozi wa Wilaya ya Kasulu kwa kubuni mkakati endelevu wa kuinua elimu wilaya humo na kuwataka kusimamia swala hilo kwa vitendo.
WAZIRI wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Profesa Joyce Ndalichako, na Mkuu wa Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma Kanali Martin Mkisi wakikagua miundombinu ya Chuo cha Elimu ya Taifa Kasulu
WAZIRI wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Profesa Joyce Ndalichako, na Mkuu wa Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma Kanali Martin Mkisi wakikagua ufanyaji wa mitihani ya Darasa la saba 2016 katika Shule ya Msingi Mwenge, Kasulu.
WAZIRI wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Profesa Joyce Ndalichako na Mkuu wa Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma Kanali Martin Mkisi wakikagua ufanyaji wa mitihani ya Darasa la saba 2016 katika Shule ya Msingi Mwenge, Kasulu.
WAZIRI wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Profesa Joyce Ndalichako akiskiliza taarifa ya elimu kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma Kanali Martin Mkisi wakati wa ziara ya mkoa wa huo leo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...