Na Humphrey Shao, Blog ya Jamii
MKUU wa Wilaya ya Ilala Mhe. Sophia Mjema (pichani) amepiga marufuku ukusanywanji wa ushuru wa biashara katika soko jipya la Pugu Kigogo fresh jijini Dar es salaam.
Akizungumza wakati ya ziara yake katika Kata ya Pugu na Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam , Mjema alichukua hatua hiyo mara baada ya kusikiliza kero za Wafanyabiashara na Wananchi wa eneo hilo ambao walifika kumsikiliza katika mkutano uliofanyika Sokoni hapo.
“Hapa kuna mambo mengi yanapswa kushughulikiwa hili pawe sawa hivyo Halamsahauri nawapa muda wa miezi mitatu wakurekebisha utaratibu huo hivyo kwa kipindi chote hicho ni marufuku kukusanya pesa kutoka katika soko hili mpaka hapo miundombinu mtakapo iweka sawa”amesema Dc Mjema.
Aliongeza kuwa ni wajibu wa Halmashauri kutengeneza mazingira mazuri hili kuweza kurahisisha ufanyikaji wa biashara wenye tija ambao autarishi afya za watu na Mazingira kwa ujumla. 
Katika hatua nyingine mkuu huyo wa Wialya amefuta vikundi vyote vya ulinzi shiriki vya kata ya Pugu kwa kumtaka OCD wa kituo cha Staki Shari kusimamia agizo hilo hili kuweza kusuka upya mfumo wa ulinzi katika eneo kutokana malalamiko ya Wananchi wa kata hiyo
Amesema kuwa wakazi wa kata ya Gongolamboto awana imani kabisa na vikundi vya ulinzi shirikishi vilivyopo katika eneo hilo ndio maana anataka ufanyike utaratibu upya kwa mujibu wa katiba amabo utawasaidia kupata vijana walio waminifu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...