Kituo cha EFM kimeendelea na harakati zake za kuwasaidia na kuwainua vijana wanaojihusisha na muziki. Kwa kutumia shindano maalumu la singeli michano linalofanyika kila siku ya jumamosi kuanzia saa nne hadi saa sita mchana, EFM radio inasaka wasanii chipukizi wenye vipaji vya kuimba nyimbo za singeli na baadae kuwaendeleza katika muziki huo. 

Zoezi hili ni endelevu na litadumu kwa muda wa wiki 12 katika maeneo mbalimbali ya Dar es salaam na Pwani ambapo muziki mnene utafika.

Jumla ya wasanii 5 huibuka na ushindi na washindi hawa hupatikana kila eneo ambapo zoezi hili la kusaka vipaji vipya vya singeli (Singeli Michano) hufanyika.

Meneja matukio na mawasiliano ya efm redio Neema Mukuarsi amesema baada ya zoezi hili wasani hawa chipukizi watapata nafasi ya kupata semina kutoka kwa TCRA, BASATA na TRA pale Dar live siku ya ijumaa ya tarehe 14.10.2016 saa 8;00 mchana ili waweze kupata elimu ya kulipa kodi,waweze kuimba nyimbo zenye maadili na kuhakikisha nyimbo zao zinakuwa na maadili katika jamii. 

Msaani chipukizi, Jfari Salumu a.k.a Winnero akionesha uwezo wake jukwaani katika tamasha la kusaka vipaji vya kuimba nyimbo za singeli jijini Dar es Salaam.
Msaani chipukizi,Ramadhani Iddi a.k.a Sindano Simba akionesha uwezo wake jukwaani katika tamasha la kusaka vipaji vya kuimba nyimbo za singeli jijini Dar es Salaam.
Mashabiki wa mziki wa nyimbo za singeli wakiendelea kupagawa katika tamasha la kusaka vipaji vya kuimba nyimbo za singeli jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...