Katibu Mkuu wa Wizara
ya Nishati na Madini Profesa Justin
Ntalikwa (mbele) akiongoza kikao cha kwanza cha kamati ya maandalizi ya mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi
kutoka Hoima nchini Uganda hadi katika
bandari ya Tanga nchini Tanzania. Kamati hiyo inajumuishwa na wawakilishi kutoka Wizara ya
Nishati na Madini, Wizara ya Ardhi,
Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wizara ya
Fedha, Mamlaka ya Mapato Tanzania
(TRA) na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (CAG). Lengo la kikao hicho ni kujadili
maandalizi ya ujenzi wa bomba
hilo.
Mratibu Miradi
ya Ubia wa Sekta Binafsi na Umma (PPP),
Salum Mnuna kutoka Wizara ya Nishati na Madini (kulia) akielezea
maandalizi ya ujenzi wa mradi wa bomba
la mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi
Tanzania katika kikao hicho. Kushoto ni Mjiolojia Mkuu kutoka Wizara
hiyo, Adam Zuberi.
Sehemu ya wajumbe wa
kikao hicho wakifuatilia maelekezo yaliyokuwa yanatolewa na Katibu Mkuu wa
Wizara ya Nishati na Madini Profesa Justin Ntalikwa (hayupo pichani) katika
kikao hicho.
Sehemu ya wajumbe wa
kikao hicho wakifuatilia maelekezo yaliyokuwa yanatolewa na Katibu Mkuu wa
Wizara ya Nishati na Madini Profesa Justin Ntalikwa (hayupo pichani) katika
kikao hicho.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...