Klabu ya Rotary ya Oyster Bay ya jijini Dar es Salaam imekabidhi rasmi ukuta uliojengwa na klabu hiyo katika Shule ya Msingi ya Msasani A na Msasani B. Ukuta huo umejengwa ili kuimarisha usalama kwa wanafunzi wa shule hizo pamoja na kulinda mali za shule. Kabla ya ujenzi wa ukuta huo, mazingira ya shule hizo yalikuwa hatarishi kwa wanafunzi kutokana na watu wasiohusika kupita katika eneo la shule bila udhibiti.

Ujenzi wa ukuta huo wenye thamani ya takribani Tshs Milioni 35 umewezeshwa na fedha zilizopatikana kutoka kwenye mojawapo ya shughuli za uchangishaji fedha zinazofanywa na klabu hiyo ambapo wadau mbalimbali walichangia ili kufanikisha zoezi hilo.

Ukuta huo ni muendelezo wa jitihada mbalimbali zinazofanywa na Klabu ya Rotary ya Oyster Bay katika kuboresha mazingira ya shule hiyo. Jitihada nyingine zilizofanyika ni pamoja na ujenzi wa maktaba mbili pamoja na kuweka vitabu vya aina mbalimbali, maji safi na salama ya kunywa, kambi ya siku moja ya huduma za bure za upimaji na matibabu ya magonjwa mbalimbali, mafunzo kwa walimu pamoja na upandaji wa miti.

Hafla hiyo fupi ilihudhuriwa na wanachama wa klabu ya Rotary ya Oyster Bay pamoja na viongozi wa ngazi ya juu wa Muunganiko wa Klabu za Rotary katika nchi za Tanzania na Uganda. Kiongozi Mkuu wa mkusanyiko wa klabu za Rotary Tanzania na Uganda, bwana Jayesh Asher alikuwa mgeni rasmi katika makabidhiano hayo na alipongeza juhudi za klabu ya Oyster Bay katika kusaidia shule hizo.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...