Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii,Mkuranga 

MBUNGE wa Mkuranga, Abdallah Ulega, amezindua kisima katika Shule ya Msingi Lupondo, kilichojengwa na African Reflection Foundation. 

Akizungumza Mara baada ya kuzindua Kisima hicho, amesema kuwa kijiji cha Lupondo kilikuwa na changamoto ya maji kwa muda mrefu. Amesema kuwa wananchi hao walikuwa wakitafuta maji umbali wa kilomita tano na kufanya kuumiza kichwa katika kuwapata wafadhili wa mradi huo. 

Ulega amesema katika kipindi cha miezi tisa ameweza kupata miradi ya maji katika vijiji sita na kuahidi kuendelea kutafuta miradi ya maji katika vijiji vilivyosalia.Hata hivyo katika uzinduzi huo Mh.Ulega ametoa msaada wa mifuko 10 ya saruji katika msikiti wa kijiji hicho. 

Nae mratibu wa African Reflection foundation, Shiraz Mohamed, amesema wataendelea kufadhili miradi ya maji katika vijiji vyenye changamoto hiyo. 
Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega,(katikati) akikata utepe wa uzinduzi wa kisima jana katika kijiji cha Lupondo.
Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega, akiwa katika picha ya pamoja na wananchi wa kijiji cha Lupondo jana mkoa wa Pwani
Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega, akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Lupondo kabla ya uzinduzi wa kisima cha maji katika kijiji cha Lupondo jana mkoa wa Pwani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...