Mkuu wa wilaya ya Iringa Mh Richard Kasesela akiongea leo na umoja wa wamiliki wa Daladala Wilayani Iringa katika ukumbi wa Siasa na kilimo kujadili changamoto mbalimbali zinazowakabiri.
Na Mathias Canal
Mkuu wa wilaya ya Iringa Mh Richard Kasesela amekutana na umoja wa wamiliki wa Daladala Wilayani Iringa katika ukumbi wa Siasa na kilimo kwa lengo la kujadili changamoto mbalimbali zinazowakabiri.
Wakizungumza mbele ya Mkuu wa wilaya hiyo Baadhi ya madereva na Makondakta
wameomba kurudishwa katika Stendi ya Miyomboni kama ilivyokuwa hapo
awali wakidai kuwa eneo la walilohamishiwa kwa sasa la Mashine tatu ni finyu na lina msongamano
mkubwa wa watu jambo ambalo ni hatari kwa usalama wa wananchi.
Dc Kasesela
amesema kuwa kurudi katika standi ya Miyomboni ni jambo lisilowezekana
kutokana na eneo hilo kuwa dogo na limezungukwa na makazi ya
watu pamoja na majengo makubwa ya biashara jambo ambalo linafanya eneo hilo kuwa hatarishi
zaidi kama iwapo kunaweza kutokea janga la moto.
"Unajua Miyomboni ni
padogo sana pia pamejibana sasa kama ikitokea moto umewaka pale ni ngumu
sana kupafikia kwa wepesi lakini pia Watu wa zima moto ndio
waliopendekeza kuwa kituo kile kihamishwe sasa nadhani mnafahamu kuwa
sheria ya zimamoto huwa ni ngumu kuipinga", alisema Mhe. Kasesera.
Lakini pia
amewataka madereva kuacha kutumika kisiasa kwani wanaofanya hivo
wanafanya kwa maslahi yao binafsi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...