Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii
MSANII wa Muziki wa Bongo Fleva kutoka kundi la Wanaume Family Chege Chigunda , leo ameadhimisha siku yake ya kuzaliwa kwa kutembelea hospitlai ya Rufaa ya Temeke na kugawa zawadi mbalimbali katika wodi ya Watoto waliozwa hapo kutokana na matatizo mbalimbali.
Akizungumza na Mwandishi wa blog hii Mapema leo Hospitalini hapo chege alisema kuwa imekuwa tofauti sana kwa watu kupenda kusheherekea katika nyumba za starehe lakini yeye ameamua kukaa na watoto hao wagonjwa hili kurudisha kile ancho kipata kwa jamii.
“Chege Chigunda amezaliwa leo hivyo ndio maana nipo hapa mtoto wa Mama Said kusherekea siku yangu ya kuzaliwa na wagonjwa kwa kutoa zawadi mbalimbali kama mnavyoziona Pampers , Dawa za Mswaki na Dawa kwa ajili ya wagonjwa ambao awana uwezo wa kujijinunuli a hivyo katika siku ya leo wamepata fursa ya kununuliwa madawa na mimi” anasema Chege.
Anasema kuwa maisha yamebadilika sana na inapaswa watu kurudi nyuma na kufanya yale yaliyoa mazuri yanayompendeza Mungu kwa kusheherekea siku zao za kuzaliwa na watu ambao wanamatazo na wenye uhitaji hili kuweza kuwapa faraja ambayo wakuwa wameikosa kwa muda kutokana na matatizo yaliyowakuta.
Alimaliza kwa kutoa wito kwa wasanii na watu maharufu kuwa na utamaduni wa kuwakumbuka watu wenye mahitaji mablimbali kila wanapopata nafasi na kiasi kidogo kwani kutoa akuhitaji kuwa na utajiri mkubwa bali ni moyo tu.
Msanii wa Muziki wa kizazi kipya kutoka kundi la Wanaume Family, Chege Chigunda akiweka sawa baadhi ya zawadi alikuwa ameziandaa kwa ajili ya Wagonjwa Temeke Hospitali.
Chege Chigunda na baadhi ya Wasanii kutoka kundi la Mkubwa na Wanawe wakielekea wodini
Chege Chigunda akitoa baadhi ya Zawadi kwa wagonjwa
Mhe Temba akiingia wodini kupeleka zawadi kwa Wagonjwa
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...