Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akifuatana na Kaimu Mkurugenzi Mkuu,pia Mkurugenzi wa Viwanja vya Ndege Zanzibar Nd,Juma Saleh (katikati) na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa,Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ,pia Kaimu Waziri wa Mawasiliano na Usafirishaji Mhe,Haji Omar Kheir(kushoto) jana alipotembelea Kituo cha Idara ya Zimamoto katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume akiwa katika ziara maalum pamoja na kuangalia eneo lililotengwa kujengwa Ofisi ya Ziama Moto katika Uwanja huo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akizungumza na Viongozi mbali mbali wakati alipotembelea eneo lililotengwa kujengwa Ofisi ya Ziama Moto katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume jana,akiwa katika ziara maalum ambapo ametoa agizo la miezi miwili kumalizika kwa ujenzi wa Ofisi za Zimamoto kwa Uongozi wa Idara hiyo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein (kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Kamishana wa Idara ya Zima Moto Zanzibar Ali Abdalla Malimosi(katikati) wakati alipotembelea eneo lililotengwa kujengwa Ofisi ya Ziama Moto katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume jana.
[Picha na Ikulu.]05/10/2016.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...