Marehemu Advocate Yusta Msoka enzi za uhai wake.
Jumuiya ya wanafunzi kutoka Shule ya msingi Changa na Shule ya sekondari Usagara zilizopo mkoani Tanga pamoja na Chuo kikuu cha Dar es salaam tunasikitika kutangaza kifo cha aliyewahi kuwa mwanafunzi mwenzetu Marehemu Advocate Yusta Msoka kilichotokea Majuzi hapa Dar es salaam.
Sisi kama wanajumuiya wenzake kupitia shule mbalimbali tulizopitia tunatoa pole zetu kwa pacha mwenzake Mwanasheria Felista Msoka na wana familia kwa ujumla, tunaungana nao pamoja katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.
Taarifa kutoka kwa familia ya marehemu zinasema mazishi yanatarajiwa kufanyika kesho tarehe 17/10/2016 hapa jijini Dar es salaam katika makaburi ya Chamanzi - Mbagala ambako ni jirani na wazazi wake wanapoishi huko Mbagala kuanzia saa 5 asubuhi kwa kutanguliwa na Chakula/ Ibada kisha kuishiwa na Mazishi katika nyumba yake ya Milele.
Kwa wale wote ambao watapata taarifa hii tunaomba umjulishe na mwingine ili tuweze kuungana pamoja kumsindikiza mwenzetu. a
BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA
JINA LAKE NA LIHIMIDIWE
AMIN.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...