Kiongozi Mkuu wa kampuni ya Simtank, Alpesh Patel (kulia) Akiwa kwenye picha ya pamoja na washindi wa shindano hilo pamoja na wafanyakazi wa Simtank.
Kiongozi mkuu wa kampuni ya Simtank, Alpesh Patel (kulia) akimkabidhi funguo ya pikipiki Ravil Patel wakati wa ugawaji wa zawadi kwa washindi wa shindano la Simtank uza ushinde.
Kiongozi Mkuu wa Kampuni ya Simtank, Alpesh Petel(Kulia) akimkabidhi ufunguo wa pikipiki Shabbir Suleiman wakati wa makabidhiano ya washindi wa shindano la Smtank uza ushinde jijini Dar es Salaam.
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
SHINDANO la SIMTANK uza ushinde limefikia tamati kwa washindi watano kupatiwa zawadi zilizokuwa zimeandaliwa kwa washiriki kufikia malengo ya mauzo, ulipaji kwa wakati na uaminifu.
Akizungumza na waandishi wa habari, Kiongozi Mkuu wa Simtank Alpesh Patel amesema kuwa muda huu ni muhimu sana kwa kuwapongeza wateja wetu ambao wamefanya vizuri katika kutengeneza daraja baina ya bidhaa zetu na jamii.
Patel amesema, kwa uhakika Simtank kwa namna yoyote imegusa maisha ya wauzaji na wake wanaotumia katika jamii kwani ni namba moja katika kipengele cha kuhifadhi maji kutokana na utumiaji wa malighafi bora kabjsa za viwango vya kufungia bidhaa za chakula na zilizoweza kuhimili mwanga wa jua.
Shindano hilo lililoanza June 1 na kumalizika Agosti 31 lilifanikiwa kupata washindi watano kwa kuangalia kipengele cha nne na kila mmoja kupatiwa pikipiki baada ya kufanyika kwa promosheni hiyo.
Washindi wa shindano hilo ni Mohamed Mohamed, Bulk Distributors Ltd, Mwanza Huduma, Shangwe Hardware Ltd na Aim Steels na Patel kuzitaka kuendelea na kauli mbiu ya kujenga mahusiano imara baina yao na wadau wa biashara.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...