Na: Geofrey Tengeneza
Bodi
ya Utalii Tanzania (TTB) imemtaka kijana wa kitanzania ambaye pia ni
mchezaji wa mpira wa kikapu Underson Simon (19) kuitangaza Tanzania na
vivutio vyake vya utalii nchini Marekani kwa lengo la kuvutia watalii
wengi zaidi kuitembelea Tanzania.
Underson
ambaye ni tunda la kituo cha Michezo cha Jakaya Mrisho Kikwete Youth
Park cha jijini Dar es salaam amepata udhamini wa masomo kwenda kusoma
shahada ya kwanza ya sayansi ya Kompyuta katika Chuo Kikuu cha Georgia
University kilichoko Atlanta Georgia nchini Marekani.
Akizungumza
wakati wa kumuaga Underson ofisini kwake jijini Dar esalaam, Mkurugenzi
Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii Tanzania Bibi Devota Mdachi mchezaji huyo
anayechipukia wa mpira wa kikapu nchini anayechezea timu mpira wa
kikapu ya vijana (vijana Busketball Club) pamoja na kumtaka ajitahidi
katika masomo yake, lakini pia amemtaka atumie fursa hiyo na ile ya
kushiriki katika mashindano mbalimbali akiwa na timu yake ya chuo kikuu
cha Georgia katika mchezo wa kikapu kuvitangaza vivutio vyetu vya
utalii.
“
Peperusha vema bendera ya nchi yetu na tumia kila jukwaa utakalopata
ikiwa ni pamoja na mitandao ya kijamii kuitangaza Tanzania kama eneo
bora la utalii duniani” alisema Bi Mdachi na kuongeza kuwa TTB
inakusudia kuanza mchakato wa kumpa heshima ya kuwa Balozi wa heshima wa
Utalii wa Tanzania.
Mkurugenzi
huyo wa TTB alimkabidhi mchezaji huyo wa mpira wa kikapu nchini,
bendera ya Taifa na vielelezo kadhaa vinavyoelezea utalii wa Tanzania
ili visaidie kumjengea uelewa zaidi kuhusu vivutio vya utalii vya
Tanzania.
Kwa
upande wake kijana huyo Underson Simon alielezea kufurahishwa kwake
kupata nafasi hiyo lakini pia kutambuliwa na TTB kama mmoja wa
wanamichezo wa kitanzania wanaoweza kuvitangaza vema vivutio vyetu vya
utalii nje ya nchi na hivyo kuchangia kukuza sekta ya utalii.
Naye
mwalimu mwandamizi (kocha) wa mpira wa kikapu wa kituo cha Jakaya
Mrisho Kikwete Bw. Bahati Mgunda amesema kituo chake kinajivunia
mafanikio hayo ya mmoja wa wachezaji wao kupata ufadhili huo wa masomo
ambao umetokana hasa na umahiri wake katika mchezo huo.
Simon
ameondoka saa 9.00 alfajiri ya leo kwa shirika la ndege la Uturuki
kuelekea nchini Marekani tayari kujiunga na chuo kikuu hicho cha
Georgia.
Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania Bi Devota Mdachi akimkabidhi Underson Simon bendera ya Taifa ishara ya kumtaka akaitangaze vema Tanzania nchini Marekani.
Underson Simon (wa pili kulia) katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa TTB Bi devota Mdachi (wa pili kushoto) na baadhi ya maafisa aliofuatana nao katika ofisi za TTB muda mfupi baada ya kukabidhiwa bendera ya Tanzania na vielelezo mbalimbali vya utalii.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...