Mkuu wa mkoa wa Morogoro Mhe. Dkt Kebwe Stephen Kebwe akipokewa na mkuu wa kitengo cha Kuboresha usalama wa jamii ( DCP) Godluck Mongi alipokwenda kufungua mafunzo ya upelelezi kwa askari wa polisi 100. ( katika ni mkuu wa mafunzo wa Jeshi la Polisi DCP Ally Lugendo. Mafunzo hayo yanafanyika katika chuo cha polisi kidatu yamefadhiliwa na Tasisi ya Hanns Sidel. Picha na Tamimu adam- Jeshi la Polisi.
Mkuu wa mkoa wa Morogoro Mhe. Dkt Kebwe Stephen Kebwe( katikati) akiimba wimbo wa maadili wa ofisa wa Polisi wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa mafunzo ya upelelezi yanayofanyika katika chuo cha polisi kidatu. Mafunzo hayo kwa askari 100 yamefadhiliwa na Taasisi na Hanns Sidel.
 (picha na Tamimu Adam – Jeshi la Polisi)

Na. Tamimu Adam - Jeshi la Polisi
Mkuu wa mkoa wa Morogoro mhe. Dkt Kebwe Stevin kabwe amesema Jeshi la polisi Tanzania ni kioo kwa majeshi ya polisi yalipo Afrika mashariki na hata afrika kwa ujumla kutokana na umahili wake wa kutoa mafunzo mbalimbali ya uaskari kwa baadhi ya nchi zilizopo afrika mashariki .

Dkt Kebwe aliyasema hayo wakati wa uzinduzi wa mafunzo ya miezi miwili ya upelelezi katika chuo cha Polisi kidatu yaliyofadhiliwa na Taasisi ya Hanns Sidel kwa askari polisi 100 waliotoka katika mkoa wa kipolisi kinondoni ambalo wamechaguliwa kwa ajili ya kutekeleza kwa weledi mpango wa kuborewsha usalama wa jamii unaoendelea kutekelezwa katika mkoa huo wa kipolisi.

“Huwezi kwenda kujifunza katika nchi ambayo haifanyi vizuri, na ndioo maana nchi za jirani huja Tanzania kwa ajili ya kujifunza namna Jeshi la Polisi Tanzania linavyo weza kuimarisha usalama wa raia na mali zao” alisema Dkt Kebwe.

Aliwataka askari hao wanafunzi wa upelelezi kujifunza kwa makini ili kuboresha umahiri walionao katika kufanikisha upelelezi ili kuweza kuleta mabadiliko ya kivitendo katika mkoa wa kinondoni kama eneo la mfano na hatimaye maboresho hayo yaweze kuenea na kutekelezwa katika mikoa yote nchini hivyo kuimarisha usalama wa raia na mali zao.
Kusoma zaidi bofya HAPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...