Idadi ya Wataalamu wa Sayansi imekuwa ikikua kwa kasi kutokana na sekta hiyo kuwa chanzo cha maendeleo na ugunduzi na kufanya kupata maendeleo.

Hayo yamesemwa na Mkuu na Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda wakati wa hafla ya Kukabidhiwa Madawati yenye thamani ya Sh. milioni 20 kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Elimu ya Shule za Al Muntazir, Azim Dewj .

"Nimeomba sana wazazi kuhamasisha watoto wao kusoma sayansi, ukifanikiwa kwenye hayo masomo sio kwamba tu utaajiriwa lakini utaajiriwa sehemu unayoitaka kutokana na ajira kuwa nyingi ukitofautisha na masomo tuliyosoma sisi,"amesema Makonda.

Nae Mwenyekiti wa Bodi ya Elimu ya Shule za Al Muntazir,Azim Dewji amesema ‘’tumeona litakuwa jambo la busara kama tutaunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano tano inayoongozwa na Rais dk. John Pombe Magufuli ambaye pia alikuwa mwalimu.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam,Paul Makonda akikata utepe kwenye hafla ya kukabidhiwa wadawati leo jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam,Paul Makonda akikabidhiwa madawati na Mwekiti wa Bodi ya Elimu ya Shule za Al Murtazir Azim Dewji ili kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambae pia alikuawa mwalimu Mh.John Pombe Mgufuli.

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda akizungumza kwenye hafla ya kukabidhiwa madawati yenye tahamani ya Sh. Milioni 20 yaliyotolewa na shule za Al Murtazir, ikiwa ni kuunga mkono kampeni ya Mkuu wa Mkoa huyo kuhakikisha watoto wote wanakaa kwenye madawati leo jijini Dar es Salaam.

Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum akizungumza machache kwenye hafla ya kukabidhi Madawati yenye jumla ya thamani ya milioni 20 yaliyotolewa na shule za Al Murtazir, ikiwa ni kuunga mkono kampeni ya mkuu wa mkoa huyo kuhakikisha watoto wote wanakaa kwenye madawati leo jijini Dar es Salaam.


Sehemu ya wazazi na wanafunzi wa Shule ya Al-Mutanzil leo jijini Dar es Salaam.Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamiii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...