Tanzania, 22nd Novemba 2016 –Agence Française de Développement (AFD) na BANK OF AFRICA- Tanzania leo wametia saini mkataba wa makubaliano ya kutoa mikopo kiasi cha shilingi bilioni 25.67 kusaidia uwekezaji kwenye nishati mbadala na ufanisi wa nishati.

Makubaliano hayo, yamewezesha upatikanaji wa zaidi ya dola milioni 11.84 kwa ajili ya kukopesha miradi mbalimbali iliyojikita katika nishati mbadala au kuongeza ufanisi wa upatikanaji au matumizi ya nishati hapa nchini kupitia BANK OF AFRICA.

Mkataba huo umesainiwa na ndugu Bruno Deprince ambaye ni Mkurugenzi wa Kanda wa AFD na ndugu Ammishaddai Owusu-Amoah, Mkurugenzi Mtendaji na Afisa Mtendaji Mkuu wa BANK OF AFRICA, mbele ya Mheshimiwa Bi Malika Berak, Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania, Mheshimiwa Mikael Melin Programme, Meneja katika Ujumbe wa Umoja wa Ulaya kwa Tanzania na Mheshimiwa Thomas Richard, Mwakilishi wa Shirikisho la Viwanda nchini (CTI).
Kutoka kushoto ni Bw. Youssef Benrhafiane Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Mikopo na Udhibiti wa BANK OF AFRICA- Tanzania, Bw. Amishadai Owusu- Amoah Mkurugenzi Mtendaji wa BANK OF AFRICA- Tanzania, HE Malika Berak, Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania, Bw. Bruno Deprince Mkurugenzi wa Kanda wa AFD Afrika Mashariki na Bw. Thomas Richard, Mwakilishi wa Shirikisho la viwanda Tanzania.

Katika makubaliano hayo, taasisi zote mbili zimethibitisha kushirikiana kupitia mpango wa SUNREF (Matumizi Endelevu ya Maliasili na Nishati). Mpango huu bunifu utaiwezesha BANK OF AFRICA kutoa mikopo ya muda mfupi na mrefu itakayowavutia sekta ya umma na binafsi kutekeleza miradi katika nishati mbadala na ufanisi wa nishati, ambayo imekuwa ikipata changamoto katika upatikanaji wa mikopo.

Mpango huu ubunifu itawezesha BANK OF AFRICA kutoa mikopo ya muda mfupi na mrefu klatika viwango vya riba nafuu kulinganisha na viwango vya kawaida vya kibiashara kwa lengo la kuwawezesha wateja katika sekta binafsi na umma, kuondokana na changamoto ya upatikanaji wa fedha za kutekeleza mpango wa nishati mbadala.
Kutoka kushoto ni Bw. Amishadai Owusu-Amoah Mkurugenzi Mtendaji wa BANK OF AFRICA-Tanzania akisaini mkataba na Bw. Bruno Deprince Mkurugenzi wa Kanda wa AFD Afrika Mashariki.

BOFYA HAPA KWA HABARI KAMILI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...