Na. Immaculate Makilika - MAELEZO

BARAZA la Madiwani ya Halmashauri ya Mji wa Bunda limemfukuza  kazi  Bw. Eliud Haonga aliyekuwa mtumishi wa Idara ya Ardhi na Mipango  na Mthamini  daraja la pili mapema wiki hii, baada ya kughushi nyaraka ili kujipatia fedha za malipo ya pango.

Bw. Haonga alipokea fedha za malipo ya pango kiasi cha shilingi milioni saba kutoka kiwanda cha OLAM Tanzania mwezi Juni mwaka huu.

Akizungumza kwa njia ya simu,  Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bunda, Mkoa wa Mara, Bi. Janeth Mayanja alisema kuwa Bw. Haonga amekiuka Sheria za Utumishi wa Umma, kanuni ya 42 na uamuzi uliotolewa na baraza la madiwani  ni sahihi.

Bi. Janeth alisema “Bw. Eliud Haonga alihifadhi shilingi milioni mbili tu katika akaunti ya Halmashauri ya Mji wa Bunda  na kutumia shilingi milioni tano kwa matumizi yake binafsi”.“Maamuzi haya yamechukuliwa baada ya Kamati ya Uchunguzi  kumaliza kazi yake kwa mujibu wa  Sheria, kanuni na taratibu za Utumishi wa Umma.” alisema  Bi. Mayanja.

Aidha,  Bi. Mayanja amewaasa watumishi wa Halmashauri  Bunda  kujiepusha na vitendo vinavyoashiria wizi na ubadhirifu,  na hatua kali  zitachukuliwa kwa yeyote atakayekiuka maadili ya utumishi wa umma.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bunda, mkoa wa Mara Bi. Janeth
Mayanja akiwa Ofisini kwake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...