Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO.

Mkuu wa Wilaya ya Chato iliyopo mkoani Geita, Shaban Ntarambe amekiri kuwa ushirikiano wa shirika la Plan International katika kudhibiti ajira hatarishi za watoto umefanikiwa kumaliza tatizo hilo katika Kijiji cha Msasa.

Hayo yamesemwa leo mkoani Geita na Mkuu huyo alipokuwa akiongea na mwandishi wa habari hii juu ya mchango wa Mradi wa Uondoaji Ajira Hatarishi na Vitendo vya Ukatili kwa Watoto unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD) na kuratibiwa na shirika la plan International jinsi ulivyowasaidia wananchi wa Kijiji hicho.

Ntarambe amesema kuwa ushirikiano wa Shirika hilo, jamii pamoja na uongozi wa migodi iliyopo kwenye Kijiji hicho umesaidia katika kuhakikisha elimu ya ajira, afya na usalama kwa watoto inatolewa, hivyo kupitia elimu hizo wananchi wamepata uelewa juu ya athari za ajira za watoto na kujumuika katika uzuiaji wa ajira hizo.

“Tumefanikiwa kwa asilimia zote kuzuia ajira za watoto katika eneo hilo ambalo lina mkusanyiko mkubwa wa wachimbaji wa madini, kimsingi ni kwa sababu ya ushirikiano unaotolewa na shirika la Plan International kwani wanatoa rasilimali nyingi zinazowezesha kufanikisha kuondoa tatizo hilo”, alisema Ntarambe.
Mkuu wa Wilaya ya Chato iliyopo mkoani Geita, Shaban Ntarambe akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya umuhimu wa Mradi wa Uondoaji Ajira Hatarishi na Vitendo vya Ukatili kwa Watoto unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD) na kuratibiwa na shirika la plan International.
Mratibu wa Mawasiliano wa Shirika la Plan International, Raymond Kanyambo akitoa shukrani kwa Mkuu wa Wilaya ya Chato, Shaban Ntarambe kwa kutambua umuhimu wa Mradi wa Uondoaji Ajira Hatarishi na Vitendo vya Ukatili kwa Watoto unaoratibiwa na shirika hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...