GLOBAL Education Link (GEL) imepeleka wanafunzi 50 ikiwa ni awamu ya tatu kwa mwaka huu hiyo inatokana na uhitaji wa wataalam katika udaktari na uhandisi.

Akizungumza wakati wa safari hiyo ya wanafunzi hao, Mkurugenzi Mtendaji wa GEL, Abdulmalik Mollel amesema nafasi ya udahili nchini ni chache hivyo kama wakala wa vyuo vya nje kuchukua nafasi kwa wanafunzi wanaokosa udahili.Amesema mwitikio wanafunzi kusoma nje ni mkubwa ikilinganishwa na miaka ya nyuma.

Mollel amesema kutokana na nchi kuingia katika sekta ya Viwanda wanafunzi wengi wamekwenda kusoma uhandisi wa Viwanda ili waweze kuja kuleta utaalam huo na nchi iweze kupata maendeleo

Amesema GEL inachofanya ni kuhakikisha wanafunzi wanaosoma vyuo vya nje kuwa wazazi wanaweza kumudu gharama za vyuo sawa na vya ndani.Hata hivyo amesema bado wanafunzi wanasajili hivyo wazazi wenye nia ya kutimiza ndoto za watoto wawasiliane na ofisi za GEL.
Mkurugenzi Mtendaji wa GEL, Abdulmaliki Mollel akiwa na wafanyakazi katika uwanja wa ndege wa Kimataifa Mwalimu Julius Nyerere.
Wanafunzi wakiingia katika chumba cha ukaguzi katika uwanja wa ndege wa Kimataifa Mwalimu Julius Nyerere.


Mkurugenzi Mtendaji Global Education Link (GEL), Abdulmaliki Mollel akizungumza na wazazi waliowasindiza wanafunzi wanaokwenda kusoma vyuo vya China.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...