Naibu Waziri Wa Afya ,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Hamis Kigwangalla akikagua baadhi ya pombe kali katika moja ya duka alilolikamata lililopo mwenge Dar es salaam wakati wa msako zidi ya watengenezaji pombe kali ambazo ni feki unaoendelea nchini. 
Naibu Waziri Wa Afya ,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Hamis Kigwangalla katikati akimuhoji muuza duka la pombe kali ambazo ni feki lilopo Manzese Dar es salaam wakati wa msako zidi ya watengenezaji pombe kali ambazo ni feki unaoendelea nchini.
Naibu Waziri Wa Afya ,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Hamis Kigwangalla wa kwanza kulia akiwa ameshika beseni lililojaa vizibo vya konyagi katika kiwanda feki kilichokamatwa maeneo ya sinza Dar es salaam wakati wa msako zidi ya watengenezaji pombe kali ambazo ni feki unaoendelea nchini kushoto ni Afisa kutoka TFDA.
Baadhi ya nyenzo za kutengenezea pombe kali ambazo ni feki aina ya konyagi katika kiwanda feki kilichokamatwa maeneo ya sinza jijini Dar es salaam wakati wa msako zidi ya watengenezaji pombe kali ambazo ni feki unaoendelea nchini.
Baadhi ya pombe kali aina ya konyagi na amarula ambazo ni feki zilizokamatwa katika duka la kuuza pombe kali lililopo manzese jijini Dar es salaam wakati wa msako zidi ya watengenezaji pombe kali ambazo ni feki unaoendelea nchini.




Na Ally Daud-MAELEZO 

Naibu Waziri Wa Afya ,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Hamis Kigwangalla ameongoza kikosi kazi katika msako wa Viwanda vinavyotengeneza pombe Kali feki ikiwemo viroba na zinginezo na kufanikiwa kukamata kiwanda feki kilichopo maeneo ya sinza jijini Dar es salaam.

Akiingoza msako huo Naibu Waziri Wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Dkt. Hamis Kigwangalla amesema kuwa msako huo unaofanywa na Wizara hiyo inashirikiana na Mamlaka ya Chakula na Dawa TFDA umefanikiwa kukamata kiwanda feki kinachotengeneza pombe aina ya viroba, konyagi, Smirnoff na zedi kilichopo sinza jijini Dar es salaam.

"Tunafanya msako huu kwa kushirikiana na kikosi kazi cha Serikali ili kuondoa pombe haramu zinazotengenezwa kiholela na kwa kutozingatia viwango vya ubora kwa maendeleo na Afya ya watanzania" alisema Dkt. Kigwangalla.

Aidha Dkt. Kigwangalla ameongeza kuwa katika msako huo wamefanikiwa kukamata kiwanda hicho kikiwa na nyenzo za kutengenezea pombe haramu kama vile chupa za konyagi, vifuniko, lebo, vifuko na nyenzo zingine za kutengenezea pombe hiyo haramu. 

Dkt. Kigwangalla amesema kuwa msako huo umebaini kwamba watengenezaji hao wanatumia gongo na spiriti kutengeneza pombe kali kitu ambacho ni hatari kwa afya ya watanzania hususani vijana hivyo kufanya nguvu ya taifa kupotea.

Katika msako huo pia ulifanikiwa kukamata maduka yanayouza pombe hizo maeneo ya Mwenge na Manzese jijini Dar es salaam ikiwa chini ya msambazaji Bw. Yusuf Abdul Kalambo mkazi wa Kimara ambaye anatafutwa na jeshi la polisi kwa ajili ya upelelezi zaidi. 

Aidha Dkt. Kigwangalla ameamuru wauzaji wa maduka hayo wafunge maduka yao mara moja na kushikiriwa na Polisi mpaka pale upelelezi utakapokamilika ili sheria stahiki ifuate mkondo wake aidha kulipa faini au kufutiwa leseni za biashara.Zoezi hilo la kusaka Viwanda feki vinavyotengeneza pombe kali linafanywa na Wizara ya Afya kwa kushirikiana na TFDA pamoja na jeshi la polisi ni endelevu mpaka bidhaa feki zitapotoweka nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...