JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII

TAARIFA KWA UMMA

MAADHIMISHO KITAIFA YA SIKU YA UTALII DUNIANI NA MAONESHO YA ‘’KARIBU KUSINI’’ 2016


Wizara ya Maliasili na Utalii  kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa  Mkoa wa Iringa, Mradi wa kuboresha Mtandao wa Hifadhi za Kusini mwa Tanzania (SPANEST)  pamoja na Wadau wa Sekta ya Utalii nchini watashiriki  katika Maadhimisho ya Siku ya Utalii Duniani   kwa mwaka 2016 sambamba na Sherehe za maadhimisho ya ‘’Karibu Kusini ‘’ Karibu Tanzania Southern Circuit’’  ambayo  Kitaifa yataadhimishwa   Mkoani Iringa kwenye viwanja vya  Kichangani  kuanzia tarehe 25 hadi 29 Novemba, 2016.
Lengo la maadhimisho hayo ni  kuweka uelewa kwa Jamii kuhusu umuhimu wa utalii na thamani yake ikiwa pamoja na  kuutangaza Utalii kwa kuihamasisha jamii kutumia fursa za utalii zilizopo katika kuinua uchumi wa wakazi wa Ukanda wa Kusini mwa Tanzania na Taifa kwa ujumla
Kauli Mbiu ya maadhimisho ya Siku ya Utalii Duniani kwa mwaka  2016  ni “Utalii kwa wote – wote wawezeshe’’ (Tourism for All – Promoting Universal Accessilibity). Kwa kuzingatia Kauli Mbiu hii, Serikali inatambua kuwa kuna watu wenye mahitaji maalumu kama vile walemavu, wazee na watoto ikisisitiza miundombinu rafiki, gharama nafuu kutembelea  vivutio vya utalii na gharama nafuu za usafiri ili kuhakikisha kwamba, utalii unawahusisha watu wengi zaidi kunufaika nao.
Katika Maadhimisho hayo, Wizara itakuwa na washiriki ambao ni Idara pamoja na Taasisi zake mbalimbali. Idara zitakazoshiriki ni Utalii, Wanyamapori, Mambo ya Kale na Misitu na Nyuki.
Kwa upande wa Taasisi zitakazoshiriki  ni Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Chuo cha Taifa cha Utalii, Makumbusho ya Taifa, Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Mamlaka ya Usimamizi ya Wanyamapori (TAWA) Mfuko wa Misitu Tanzania  (TaFF) Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania, (TFS)  Taasisi ya Utafiti wa Misitu na Wadau wa Wizara ya Maliasili na Utalii.
Wadau wa Sekta ya Utalii kutoka mikoa  ya Nyanda za Juu Kusini watashiriki kuonesha bidhaa na huduma zao muhimu. Mikoa hiyo ni pamoja na Iringa, Njombe, Ruvuma, Mbeya na Songwe
Aidha, Wizara itatoa punguzo kwa watanzania kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Ruaha pamoja na vivutio vya utalii vilivyokaribu na mji wa Iringa ambavyo ni Ismila,Kalenga na Boma la Mkuu wa Wilaya  kwa gharama nafuu.
Kupitia Maadhimisho hayo wito unatolewa kwa kuwaalika wadau wote wa utalii na jamii husika kwa pamoja na kuadhimisha siku hii kama ishara ya jitihada za pamoja za kuufanya utalii nguzo ya kweli ya maendeleo ya jamii na maendeleo ya jamii ni chanzo cha sekta ya utalii endelevu zaidi.
 Imetolewa na:
Kitengo cha Habari na  Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Maliasili na Utalii.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...