Na Humphrey Shao,Globu ya Jamii

Serikali imejipanga kufanyia kazi mapendekezo yaliyotolewa na jukwaa la usafirishaji nchini ,ili kuboresha hali ya usafiri hapa nchini kutoka bandarini kutoka nchini jirani.

Hayo yamesemwa na Katibu mkuu wa Wizara ya Mawasiliano na uchukuzi,Profesa Faustine Kamuzora alipokuwa akifungua jukwaa hilo lililoasisiwa na tasisi ya Trade Mark East Afrika.

"Hivyo serikali imejipanga na kuakikisha kuwa bandari ya Dar es Salaam inakuwa sehemu rafiki kwa wafanyabiashara kutoka nchi zinazotunguka kwa kupunguza urasimu unaochangia kuchelewa kwa kutoa mzigo bandarini"amesema Prof Kamuzora.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jukwaa hilo la usafirishaji ,Angelina Ngalula , amesema kuwa serikali inatakiwa kuanza kuandaa mazingira ya upatikanaji wa mzigo wa tani milioni 10 katika reli ya Standard Geji inayo taraji kujengwa hapa nchini .

Amesema kuwa wazo la serikali la kujenga reli ya kisasa ni zuri hivyo tunaiomba serikali inahakikisha inaandaa mazingira ya upatikanaji wa mizigo hili tusije tukaiona reli hiyo kama pambo tu.
  Mkurugenzi mkazi wa Trademark East Afrika,John Ulanga akizungumza na wadau wa usafirishaji wakati uzinduzi wa jukwaa lamusafirishaji.
 Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF ,Godfrey Simbeye  akito maelezo jinsi tasisi yake inavyofanya kazi bega kwa bega na wawekezaji ususani katika swala la usafirishaji.
 Mwenyekiti wa Jukwaa la Usafirishaji ,Angelina Ngalula akizungumza na wadau wa usafirishaji wakati uzinduzi wa jukwaaa hilo.
 Katibu mkuu wa wizara ya Uchukuzi,Prof Faustine Kamuzora akitoa hotuba ya ufunguzi wa jukwaa la usafirishaji jijini Dar es Salaam
Wadau wa usafirishaji wakisikiliza kwa makini wakati wa uzinduzi wa jukwaa hilo.
 Picha ya pamoja ya wadau wa usafirishaji na mgeni rasmi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...