Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Bw. Bernard Konga akiongozana na baadhi ya wakurugenzi wa Mfuko na uongozi wa Hospitali ya Kairuki walipotembelea maeneo mbalimbali ya hospitalini hapo kuangalia huduma zinazotolewa kwa wanachama wa Mfuko. Pichani akimjulia hali mwanachama wa Mfuko aliyelazwa hospitalini hapo.

Na Grace Michael

KAIMU Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Bw. Bernard Konga amezitaka Hospitali zote nchini zinazohudumia wanachama wake kuhakikisha zinatoa huduma bora na zinazostahili kwa wanachama ikizingatiwa ukweli kwamba wamekwishazilipia huduma hizo kabla ya kuugua.

Aidha amewahakikishia wanachama wa Mfuko kwamba, Mfuko umejipanga kuwahudumia na kutatua kero wanazokabiliana nazo wakati wa kupata huduma ili wajivunie huduma walizolipia.

Bw. Konga amesema hayo wakati alipofanya ziara ya kujionea namna wanachama wa Mfuko wanavyohudumiwa katika Hospitali ya Kairuki mjini Dar es Salaam ambapo mbali na kuona huduma pia alipata fursa ya kuzungumza na wanachama waliofika hospitalini hapo kupata huduma.
Bw. Konga akiwasikiliza wanachama wa Mfuko waliokuwa wakipata huduma za matibabu hospitalini hapo.

Akizungumza na wanachama katika Hospitali ya Kairuki, Bw. Konga alisema kuwa ameamua kuanza ziara ya kutembelea hospitali zote ili kukutana na wanachama, kusikiliza kero zao pamoja na kuzungumza na watoa huduma kwa lengo la kutatua matatizo yaliyopo na kujenga uhusiano bora.

“Nimeamua kuanza rasmi ziara hizi za kikazi kuwaona moja kwa moja wanachama wanahudumiwa ili nizungumze nao na kupata maoni kutoka kwao…wanachama kwangu ndio kipaumbele cha kwanza kwa kuwa ndio wametupa dhamana ya kuwahudumia na kukaa na fedha zao hivyo binafsi sitakubali kuona mwanachama akipata huduma hafifu”. Alisema Bw. Konga.

Alisema kuwa kitendo cha kutoka na kusikiliza wanachama kitasaidia kwa kiasi kikubwa kuboresha huduma lakini pia kukutana uso kwa uso na wananchi ambao Mfuko unawahudumia.
Wakiendelea kupata maelezo ya huduma hospitalini hapo.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...