TAARIFA
KWA UMMA
MAADHIMISHO YA SIKU
YA ARDHIOEVU DUNIANI TAREHE 2 FEBRUARI 2017
Kesho tarehe 2
Februari, 2017 ni maadhimisho ya siku ya Ardhioevu Duniani. Siku hii
inaadhimishwa duniani kote kwa kutoa elimu na kuwakumbusha
watu wote kuhusu uhifadhi na matumizi endelevu ya rasilimali za ardhioevu.
Ardhioevu ni maeneo
ya ardhi yaliyopo kandokando na ndani ya Chemchem, Mito, Maziwa na mwambao wa
bahari wenye kina cha maji yasiyozidi mita sita wakati wa kupwa. Ardhioevu pia
hujumuisha Madimbwi, Mabwawa, Tingatinga na sehemu zote yanapokusanyika maji
kipindi kirefu cha mwaka.
Tanzania hujumuika
na nchi nyingine wanachama wa Mkataba wa “Ramsar” kuadhimisha siku ya ardhioevu
duniani Februari 2 kila mwaka. Ujumbe wa mwaka huu wa Siku ya Ardioevu ni: "Ardhioevu
Hupunguza Athari za Majanga” (Wetlands for Disaster Risk
Reduction)".
Tafsiri ya kauli mbiu hii ni kwamba, Ardhioevu huzuia majanga
ya mafuriko yanayoweza kutokea katika pwani za bahari, hupunguza athari za
kiafya zinazoweza kujitokeza kutokana na madini hatarishi kama Zebaki,
hupunguza uwezekano wa kutokea kwa baa la njaa kwa kuwa maeneo okozi wakati wa
kiangazi kama vyanzo vya maji na chakula kwa binadamu na wanyama.
Ardhioevu pia
ni maeneo yenye uzalishaji mkubwa wa chakula kama vile mpunga na mbogamboga na
chanzo cha maji yanayotumika kwenye kilimo cha umwagiliaji nchini. Arhioevu pia
ni sekta endeshi ya uchumi wa nchi kwa kuwa ni chanzo cha maji yanayotumika
kwenye kilimo, viwandani pamoja na uzalishaji wa umeme wa maji kwa gharama
ndogo.
Inakadiriwa kuwa
asilimia 10 ya ardhi ya Tanzania ni ardhioevu ambayo ni muhimu kwa bioanwai,
uchumi, shughuli za kijamii na kiikolojia. Maeneo haya ni makazi muhimu ya aina
mbalimbali za viumbe hai wakiwemo samaki, viboko, mamba, ndege na viumbe
wengine wasio na uti wa mgongo. Katika ikolojia ya ardhioevu tunapata bioanwai
kubwa kuliko eneo lingine lolote duniani.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...