Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro leo Jumatano Machi 15,2017 amefungua mafunzo ya siku tatu kuhusu usajili wa watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga. 

Mafunzo hayo yanahudhuriwa na maafisa watendaji wa kata 26 pamoja na wasaidizi wao na watoa huduma katika vituo vya afya na zanahati zilizopo katika halmashauri hiyo. 

Mafunzo hayo yameandaliwa na Wakala wa Usajili wa Vizazi na Vifo nchini RITA kwa ufadhili wa shirika la watoto la UNICEF. 

Akizungumza wakati wa kufungua semina hiyo Matiro alisema kuanzia sasa vyeti vya kuzaliwa vya watoto vitatolewa katika ofisi ya mkurugenzi wa halmashauri badala ya ofisi ya mkuu wa wilaya ili kuwarahisishia wananchi kupata huduma hiyo. 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza ukumbini ambapo mbali na kuwahamasisha kuandikisha watoto pia aliwataka maafisa watendaji wa kata kuhakikisha kuwa watoto wote wanaotakiwa kuandikishwa shuleni waandikishwe 
Washiriki wa semina hiyo wakiwemo maafisa watendaji wa kata na watoa huduma za afya katika vituo vya afya na zahanati katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga 
Afisa Maendeleo halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Daudi Kisangure akizungumza wakati wa semina hiyo ambapo alisema .
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza na washiriki wa semina hiyo 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...