Mheshimiwa Dkt. Hamisi Kigwangalla (Mb) , Naibu Waziri wa Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto akichangia mada katika kikao cha ngazi  ya Mawaziri kuhusu uwezeshaji wa Wanawake Waliopo kwenye sekta isiyo rasmi.


Dkt. Kigwangalla ameelezea jinsi ambavyo kwa upande wa Tanzania, Serikali imepiga jitihada Kubwa kuhakikisha inamkomboa mwanamke kutoka kwenye utegemezi kwa kuunda vyombo mbalimbali na kuandaa sera na miongozo inayoelekeza usawa katika kufikia malengo ya kumkomboa mwanamke kiuchumi ambapo mwanamke anakuwa na haki na uwezo wa kukopa katika taasisi mbalimbali ili kuanzisha au kukuza mtaji wa biashara yake katika kufikia malengo aliyotarajia. 

Vile vile amesema serikali imeanzisha mfuko wa maendeleo katika halmashauri zote 114 nchini ili kuwafikia wanawake walio wengi zaidi , imeendelea kuhamasisha Jamii kuanzisha  mifuko mbalimbali ya kuweka na kukopa Kama vile (VIKOBA)  , kuwahamasisha kushiriki katika maonyesho mbalimbali ya kitaifa na hata mikutano mikubwa ya kimataifa ili kujitangaza na kukuza bidhaa mbalimbali kwa lengo la kujipatia kipato na kukuza mitaji yao.

Alisema, katika kufanya hivyo, kunawasaidia kutengeneza mitandao ya kibiashara itakayowasaidia kukua kimataifa na kufanya biashara Kubwa za kimataifa na pia kutoa ajira kwa Wanawake wenzao . Pia , Serikali imeanzisha benki ya Wanawake ambayo Kazi yake Kubwa ni kutoa mikopo na ushauri ambao utawasaidia  kukuza biashara zao na kuongeza kipato kwani Wanawake ni Jeshi Kubwa ambalo linachangia uchumi wa nchi kwa kiasi kikubwa.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...