Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba ameagiza kusitishwa mara moja kwa shughuli zote za kibinadamu kando kando ya Vyanzo vya maji.
Rai hii imetolewa leo na Waziri Makamba mara baada ya kufanya ziara ya kukagua hali ya mazingira katika Mkoa wa Pwani eneo la Mto Mpiji ambao umeathirika kutokana na Uchimbaji wa mchanga na mmomonyoko wa ardhi unaohatarisha maisha ya wakazi wa eneo hilo.
Waziri Makamba amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bagamoyo Bi. Fatuma Latu kuwaondoa watu wote waliojenga pembezoni mwa Mto Mpiji na kuhakikisha zoezi hilo linafanyika ndani ya siku 30. " Mkurugenzi hakikisheni kuwa wakazi hao waliovamia eneo la mto huu na kujenga makazi yao ya kudumu wanaondolewa mara moja" Alisisitiza Waziri Makamba.
Baadhi ya nyumba zilizopo Mpigi darajani ambazo zinatakiwa kubomolewa kutokana na kujengwa ndani ya mita sitini kutoka katika chanzo cha maji. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. January Makamba (Mb.) amegiza wenye nyumba hizo wabomoe kwa gharama zao wenye.
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. January Makamba (Mb.) akiongea na wananchi wa eneo la Mpigi darajani (hawapo pichani) na kusisitiza katazo la kufanya shughuli zozote za kibinadamu ndani ya mita sitini. Kushoto ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bagamoyo Bi. Fatuma Latu
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. January Makamba (Mb.) alipotembelea Mamlaka ya Usafi na Mazingira Chalinze kujionea changamoto za uchafuzi wa mazingira katika mto Wami.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...