Na Mwamvua Mwinyi,Kibaha

WANAFUNZI wa shule ya sekondari ya kata ya Pangani,Kibaha Mji,wanakabiliwa na adha ya kutembea umbali wa km.34 kila siku,hali inayosababisha baadhi yao kuwa watoro, kukatisha masomo na kupata mimba.

Aidha shule za msingi zilizopo katika kata hiyo,zina uhaba wa walimu ambapo shule yenye wanafunzi 950 ina walimu kumi pekee hivyo kusababisha muda mwingi wanafunzi kucheza.

Hayo aliyasema diwani wa kata ya Pangani,Agustino Mdachi,wakati alipokuwa akizungumzia changamoto za kielimu ,kwenye ziara ya mbunge wa jimbo la Mji wa Kibaha,Silvestry Koka,aliyoifanya katika kata hiyo.

Alisema,wanafunzi wanaosoma kwenye ya shule ya kata wanapata usumbufu na wapo katika wakati mgumu.
Diwani wa kata ya Pangani,Agustino Mdachi akizungumza na wananchi wa kata hiyo kwenye ziara ya mbunge wa jimbo la Kibaha Mji,Silvestry Koka aliyoifanya katika kata hiyo.
Baadhi ya wakazi wa kata ya Pangani,wakisikiliza jambo katika ziara ya mbunge wa jimbo la Mji wa Kibaha, Silvestry Koka kwenye kata hiyo.
Mbunge wa jimbo la Mji wa Kibaha ,Silvestry Koka,akizungumza jambo katika ziara yake kata ya Pangani .(picha na Mwamvua Mwinyi).


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...