Wananchi wa jamii ya wafugaji katika kijiji cha
Mbukeni,Kata ya Harashi ,tarafa ya Loliondo wilayani Ngorongoro jana wamezuia
kwa muda msafara wa kamati ya kudumu ya Ardhi,Maliasili na Utalii wakishinikiza
kusikilizwa kero zao.
Katika Pori tengefu la Loliondo
lililopo wilayani Ngorongoro mkoani Arusha kumekuwa na mgogoro uliodumu
kwa zaidi ya miaka 25 sasa huku suluhu ya utatuzi wa kiini cha mgogoro huo
kikitafutiwa ufumbuzi.
Kamati ya kudumu ya Bunge ya
Ardhi,Maliasili na Utalii imetembelea maeneo mbalimbali ya Pori hilo kwa lengo
la kujionea hali halisi kabla ya kutoa tamko juu ya mgogoro huo ambapo ikiwa
njiani kuelekea Mamlaka ya Ngorongoro ikakutana na kundi la wafugaji wakiwa
wamezuia barabara
Hatua ya wafugaji hao kusimamisha msafara
wa kamati inakuja muda mfupi baada ya kamati kufanya kikao na wawakilishi wa
wafugaji hao,kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Hotel ya Domel.
Wananchi wa jamii ya wafugaji katika kijiji cha Mbukkeni ,kata ya Harashi wakiwa wamezuia msafara wa kamai ya kudumu ya Bunge ya Ardhi,Maliasili na Utalii iliyofanya ziara kutembelea Pori tengefu la Loliondo kupata hali halisi ya mgogoro uliopo .
Wajumbe wa kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi,Maliasili na Utalii walilazimika kushuka na kuzungumza na wananchi hao.
Wajumbe wa kamati hiyo wa kuzungumza na wananchi wa jamii ya wafugaji katika eneo hilo.
Vijana wa jamii ya wafugaji wakiwa wamebeba silaha za jadi .
Mbunge wa Jimbo la Siha ambaye pi ni jummbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi,Maliasili na Utalii,Godwin Mollel akizungumza na wananchi wa jamii ya Wafugaji katika kijiji cha Mbukeni baada ya kuzia safara wa kamati hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...