Zanzibar imeshauriwa kuchangamkia furSa mbali mbali za ushirikiano
zinapokezea baina yake na Serikali za Majimbo Nchini India katika
sekta za Kilimo, Biashara, Uwekezaji, Afya na huduma za Mawasiliano
kutokana na Taifa hilo liliopo Barani Asia kupiga hatua kubwa ya
Maendeleo kwenye Sekta hizo.

Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Balozi wa Tanzania Nchini India Balozi
Mohamed Hija wakati akikiongoza Kikao cha matayarisho cha Ujumbe wa
Zanzibar unaoongozwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif
Ali Iddi ambao tayari umeshawasili Nchini humo kwa Ziara ya Kiserikali
ya Wiki Moja.

Balozi Mohamed Hija alisema Zanzibar ina fursa pana ambazo bado
haijazitumia katika kujitanua kimawasiliano kwa kushirikiana na
Taasisi mbali mbali Duniani katika harakati zake za kujikwamua
kiuchumi na kuimarisha mipango yake ya Maendeleo hasa kwenye zile
Sekta zilizo nje ya Muungano.

Alisema India imebarikiwa kuwa na Taasisi na Makampuni mengi kwenye
Serikali za Majimbo ambazo zinaweza kusaidia nguvu za Kiuchumi
Visiwani Zanzibar iwapo mipango ya uhakika itawekwa ukiwemo utaratibu
maalum wa kufuatilia makubaliano yanayofikiwa ya pande mbili husika.
Balozi Hija aliueleza Ujumbe huo wa Zanzibar kwamba Ofisi ya Ubalozi
Nchini India iko tayari kuratibu masuala yote yatayohusika na mikataba
au makubaliano baina na Zanzibar na Taasisi au Serikali ya Jimbo
lolote Nchini humokatika uanzishwaji wa ushirikiano wa kisekta.
Kaimu Balozi wa Tanzania Nchini India Balozi,Mohamed Hija kati kati akielezea fursa mbali mbali zilizopo Nchini India ambazo Zanzibar inaweza kuzichangamkia kwenye kikao cha Ujumbe wa Zanzibar uliowasili Nchini humo kwa ziara ya Wiki Moja.

Balozi Hija alikuwa akikiongoza Kikao cha matayarisho cha Ujumbe wa Zanzibar unaoongozwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi hapo kwenye Hoteli ya Kimataifa ya Eros – Nehru Palace iliyopo Mjini New Delhi India.

Wa kwanza Kulia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Bibi Asha Ali Abdulla. Wa kwanza Kushoto ni Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi ambae pia ni Waziri asiye ya Wizara Maalum Dr. Sira Ubwa Mamboya na Naibu Waziri wa Nchi
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mh. Mihayo Juma N’hunga.

Picha na – OMPR – ZNZ.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...