Balozi wa Kuwait nchini Tanzania Jasem Al-Najem amezindua kisima cha 27 katika shule ya msingi Majani ya Chai iliyopo Vingunguti ikiwa ni ka
Katika tamati ya awamu ya kwanza ya mpango wa Ubalozi wa Kuwait wa kuchimba Kisima kwa kila shule mpaka sasa kumezinduliwa visima vya maji 27 katika shule 27 mbalimbali katika kipindi cha miezi mitatu tu jijini Dar es salam.
Mpango huo wa Ubalozi wa Kuwait umeweza kufanikiwa ambapo visima 16 kati ya hivyo vilichimbwa na Jumuiya ya mwezi mwandamo ya Kuwait (Kuwait Red Crescent Society ).
Visima vingine vilichimbwa na wasamaria wema wa Kuwait kwa kushirikiana na asasi nyingine za nchin Tanzania na Kuwait.
Balozi wa Kuwait nchini Tanzania Jasem Al-Najem akizindua kisima katika Shule ya Msingi Majani ya Chai iliyopo ya Vingunguti akiwa pamoja na wanafunzi wa Shule hiyo na walimu ikiwa ni mpango wa kwanza wa ubalozi wa nchi hiyo kuchimba kisima katika Shule za Msingi Jijini Dar es salaam
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...