Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

Chuo kikuu cha shenyang kutoka nchini China kimeahidi kutoa ushirikiano na Shirika la ndege la Air  Tanzania kwa kutoa msaada wa kuwasomesha wafanyakazi wa kampuni hiyo,ili waweze kumudu ushindani wa soko la kimataifa.

Hayo yamesemwa na mwalimu wa malezi wa chuo cha Shenyang, Shi Guangda katika mkutano ulioandaliwa na Taasisi ya Global Education Link kwa wazazi ambao watoto wao wanasoma urubani na Masuala ya anga katika chuo hicho.

“Tangu Rais wetu wa China alipofika hapa tumekuwa na mahusiano makubwa na nchi hizi mbili, hivyo kwa kuanza kama chuo chetu tutatoa ufadhili kwa wafanyakazi wa shirika la ndege la Air Tanzania na kubadilishana mafunzo katika chuo cha usafirishaji cha NIT na Shenyang” Amesema Guangda .

Kwa upande wa Mkurugenzi mkuu wa shirika la ndege la Air Tanzania,Ladislaus Matindi ameishukuru tasisi ya Global Education Link kwa  kuwaunganisha na chuo hicho ambacho kwa sasa kimekuwa msaada mkubwa kwa kutoa mafunzo kwa wafanyakazi wa shirika hilo.

Matindi ametaja kuwa upatikanaji wa nafasi hiyo itasaidia kutoa motisha kwa vijana wetu ambao wanafanya kazi katika shirika hilo na wengine ambao wako nje kuwa na hamu ya kusoma masuala ya usafirishaji .

Kwa upande wake mkurugenzi wa Global Education link , AbduMalik Molell alitumia fursa hiyo kuzungumza na wazazi hao juu ya swala la bima ya wanafunzi amabo wanasoma chuo hicho katika swala zima la matibabu na majanga mengine ambayo yatawakuta wanafunzi.


Mkurugenzi wa Global Education Link, AbdulMalik Mollel akimkabidhi hati ya ufadhili wa masomo Mkurugenzi wa shirika la ndege nchini Air Tanzania,Ladislaus Matindi kwa ajili ya wafanyakazi wa shirika hilo watakotakiwa kwenda kusoma China
Mkurugenzi wa Shirika la Ndege la Air Tanzania Ladislaus Matindi akizungumza na wazazi ambao watoto wao wanasoma masuala ya Anga nchini China
Mkurugenzi wa Global Education Link, AbdulMalik Mollel akifafanua jambo kuhusu masuala ya bima ya matibabu kwa wazazi ambao wamefika katika mkutano huo
Mlezi wa wanafunzi kutoka chuo Shenyang, akizungumza juu ya mazingira na ufadhili walio utoa nchini kwa shirika la ndege.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...