Mchezaji
wa timu ya Dar City, Shadrack Nsajigwa akiondoka na huku akisindikizwa
na Mchezaji wa Timu Boko Veterans wakati wa mchezo wa kirafiki
uliochezwa kwenye Uwanja wa Boko Veterani mwishoni mwa wiki. Katika
mchezo huo Dar City ilishinda mabao 3-2, kupitia kwa wachezaji wake
Makocha Tembele na Salvatory Edward. Kikosi cha Dar City kinaundwa na
wachezaji mbalimbali waliowahi kutamba katika Ligi Kuu Tanzania miaka ya
nyuma pamoja na .
Kiungo
hodari wa Dar City, Shaffih Dauda akiwania mpira na Mchezaji wa Timu
Boko Veterans wakati wa mchezo wa kirafiki uliochezwa
kwenye Uwanja wa Boko Veterani mwishoni mwa wiki. Katika mchezo huo Dar
City ilishinda mabao 3-2, kupitia kwa wachezaji wake Makocha Tembele na
Salvatory Edward. Kikosi cha Dar City kinaundwa na wachezaji mbalimbali
waliowahi kutamba katika Ligi Kuu Tanzania miaka ya nyuma pamoja na
baadhi ya wadau wa soka na wanahabari.
Kiungo
wa Timu ya Dar City, Tippo Athuman al maarufu Zizzou ambaye ni muasisi
wa timu hiyo, akitafuta namna ya kuwatoka mabeki wa Timu ya Boko Beach
Veterans, wakati wa mchezo wa kirafiki uliochezwa
kwenye Uwanja wa Boko Veterani mwishoni mwa wiki.
Nahodha wa Timu ya Boko Beach Veterans, John Dilinga a.k.a Dj JD akiajiandaa kuachia shuti.
Makocha Tembele (katikati) akiwasakata wachezaji wa Boko Veterans, Godfrey Ngonyani (kushoto) na John Dilinga 'Dj Jd'.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...