Na
Bashir Yakub.
Kwa mujibu wa
sheria ya usajili wa
ardhi sura ya 334
ipo aina ya
mikataba ya pango
ambayo baada ya
kuwa imeingiwa kati
ya mpangaji na mwenye nyumba/eneo
ni lazima isajiliwe.
Mikataba ya aina
hiyo isiposajiliwa inakuwa
haijakidhi vigezo vya
kisheria na hivyo
kubatilika.
Aidha pango huhusisha
shughuli mbalimbali. Yapo
mapango kwa ajili
ya biashara maduka,
bar, mahoteli n.k. na pia
yapo mapango kwa
ajili ya makazi. Iwe
umepanga kwa ajili
ya biashara au
makazi madhali aina
yako ya upangaji
inahitaji kusajiliwa kisheria
basi huna budi kufanya
hivyo ili uhalali
wa pango lako upatikane.
Kabla ya kuona
aina ya mikataba
ya pango ambayo ni
lazima kusajiliwa ni
vyema kujikumbusha kidogo
kuhusu haki za
mpangaji.
1.HAKI ZA
MPANGAJI.
( a ) Haki
ya kutoingiliwa na
mwenye nyumba ili
kumpa uhuru mpangaji kufurahia pango
lake.
( b ) Haki
ya kumpa taarifa(notice) mapema
mpangaji ikiwa mwenye nyumba anataka
kukagua nyumba/eneo lake.
( c ) Haki
ya kutoondolewa au
kusitishiwa mkataba mpaka
baada ya kupewa taarifa
maalum( notice) .
( d ) Haki
ya kuambiwa ukweli
kuhusu hali ya
nyumba kabla ya kusaini
mkataba wa pango. Mfano
kuambiwa ikiwa eneo
linajaa maji kipindi
cha mvua, kuambiwa ikiwa
nyumba inavuja n.k.
( e ) Haki
ya kukataa sharti
lolote ambalo linalenga kuminya uhuru
wa mpangaji au
linalovunja sheria yoyote
ya Tanzania.
( f ) Haki
ya kupewa taarifa
mapema(notice) kabla ya
kupandisha kodi ya
pango.
( g )
Haki ya kupewa
taarifa mapema(notice) kabla
ya kubadilisha sharti
lolote katika mkataba
wa pango.
KUSOMA ZAIDI sheriayakub.blogspot.com
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...