Na Dotto Mwaibale
BARAZA la Uongozi la Dini na Amani Tanzania (IRCPT), limesema
ipo haja mchakato wa Katiba Inayopendekezwa kufikia tamati kwa kuwa
ina mambo ya msingi kwa Watanzania.
Mkurugenzi wa Baraza hilo, Mchungaji Thomas Godda amesema ni
vema viongozi wa dini wakatimiza wajibu wao kwa kuihamasisha
Serikali imalize mchakato huo sanjari na kuhamasisha wananchi kusoma
Katiba iliyopo ili kuwajengea uelewa mpana.
Ametoa kauli hiyo leo Dar es Salaam kwenye semina ya siku
mbili ya kuhamasisha uhiishaji wa Katiba Mpya kwa viongozi wa dini inayoendelea
kwenye Hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam ambayo imeandaliwa
na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC).
Aliongeza kuwa viongozi wa dini si wanaharakati bali ni watu
wanaotoa uamuzi wao kwa hekima huku wakiaminiwa na wafuasi wao wakiwemo
viongozi wa serikali.
Mkurugenzi wa Baraza la Dini na Amani Tanzania (IRCPT), Mchungaji Thomas Godda, akihutubia wakati akifungua semina ya siku mbili ya viongozi wa dini kuhamasisha uhiishaji wa katiba mpya inayoendelea Hoteli ya Golden Tulip Posta jijini Dar es Salaam leo. Semina hiyo imeandaliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC).
Mwenyekiti wa Taifa wa Wanawake wa Baraza la Kiislam Tanzania (Bakwata), Shamim Khan (kulia), akizungumza katika semina ya siku mbili ya viongozi wa dini kuhamasisha uhiishaji wa Katiba mpya iliyofanyika Dar es Salaam leo. Semina hiyo imeandaliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...