Na
Bashir Yakub
Transfer ni kubadilisha
hati au leseni
ya makazi kutoka
jina la mmiliki
wa awali kwenda kwa
mmiliki mpya. Transfer
inaweza kufanyika kutokana na mauzo, kupewa zawadi, fidia, n.k. Kwahiyo
kuzuia transfer ni
kuzuia kubadilishwa kwa
hati kutoka mmiliki wa
awali kwenda mmiliki
mpya. Mara nyingi tumezoea
kuzuia transfer kwa
kutumia mahakama ( court injuction).
Sasa yatupasa tufahamu
kuwa ipo
njia nyingine nyepesi ambayo
haihusishi mahakama. Ni
njia ya maombi
kwa kamishna wa
ardhi kwa mujibu
wa Sura ya 113
, sheria
ya ardhi ,namba 4, ya mwaka 1999
vifungu vya 38, 39
na 41 . Kabla ya kuona
ufanyeje kutumia njia
hii ni vema tuone
mazingira ambayo yakikutokea unaweza kutumia
hiyo njia.
1.HAYA YAKITOKEA
UNAWEZA KUPELEKA MAOMBI
KWA KAMISHNA.
( a ) Mme
wako au mke
wako ameuza kiwanja
au nyumba yenu
na kuna namna
ambavyo mauzo hayo
unadhani sio halali
kwasababu yoyote ile
ya kisheria pengine ya kutokushirikishwa, au
kushirikishwa lakini baadae
kunyimwa haki yako
kwa mujibu wa
makubaliano au vinginevyo. Lakini wakati
huo unadhani huna
la kufanya kwakuwa
mauzo tayari yamefanyika
na pengine hata
wewe ulishasaini.
( b ) Una
maslahi na haki
katika nyumba/kiwanja cha mirathi .
Mali hiyo imeuzwa
bila wewe kushirikishwa
au umeshirikishwa lakini
haki zako za
msingi hazikuzingatiwa au
namna nyingine yoyote
ambayo kwayo unahisi
mchakato haukwenda sawa.
Lakini wakati huo
unadhani huna la
kufanya kwakuwa mauzo tayari
yamefanyika na pengine
hata wewe ulishasaini.
( c ) Umemuuzia mtu
nyumba/kiwanja lakini amekataa
kutekeleza baadhi ya
makubaliano ya msingi yaliyo
katika mkataba wenu
wa mauziano na
sasa anafanya mchakato
wa kubadili hati.
( d ) Na mazingira mengine
yoyote ambayo tayari nyumba/kiwanja kimeuzwa
lakini ukaona kuna
haja ya kuzuia
mchakato wa kubadilishwa jina la
mmiliki ili baadhi
ya mambo yawekwe sawa kwanza.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...