Meneja Mwandamizi Kitengo cha Amana, Bima na Huduma za ziada wa Benki ya NMB, Bw. Stephen Adili (kushoto) akitoa maelezo namna benki hiyo inavyowakumbuka vijana katika bidhaa zao mbalimbali kwa wageni waalikwa, Mkurungenzi Mkuu wa UN CDF Tanzania, Peter Malika (wa kwanza kulia) na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (wa pili kulia) walipotembelea banda hilo kwenye uzinduzi wa mjadala kujadili changamoto mbalimbali na kuhamasisha vijana nchini kupata uelewa wa masuala ya fedha. Mkurungenzi Mkuu wa UN CDF Tanzania, Peter Malika (kushoto) akimkabidhi Meneja Mwandamizi Kitengo cha Amana, Bima na Huduma za ziada wa Benki ya NMB, Bw. Stephen Adili (kulia) cheti kilichotolewa na UN-CDF Tanzania, kwa NMB kwenye kampeni kuwahamasisha vijana kupata uelewa wa masuala ya fedha wakiwa ndani ya banda la Benki ya NMB kujua huduma anuai zinazotolewa na benki hiyo na kuwagusa vijana. NMB imeshiriki kufanikisha kampeni hizo. Baadhi ya wageni waalikwa katika kongamano la kampeni zilizowakutanisha vijana kujadili changamoto mbalimbali, wakipokea vipeperushi ndani ya banda la NMB kwenye kongamano hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...