....Aagiza TCU
kutowachagulia Wanafunzi wa Elimu ya Juu Vyuo.
Na Lilian Lundo na Beatrice
Lyimo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameiagiza Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU)
kutowachagulia vyuo wanafunzi wa elimu ya juu na kuwaacha wanafunzi hao
kuchagua vyuo wanavyovitaka wenyewe.
Agizo hilo limetolewa leo, Jijini
Dar es Salaam Rais Magufuli alipokuwa akizindua Mabweni mapya ya Chuo Kikuu cha
Dar es Salaam ikiwa ni ahadi yake aliyoitoa Chuoni hapo Juni, mwaka jana.
“Ninaamini kama wanafunzi
wangepewa nafasi ya kuchagua vyuo wanavyovipenda wenyewe, vyuo vya Serikali kama
vile Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA)
Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na Chuo Kikuu cha Mzumbe vingekuwa na wanafunzi
wengi sana,” alisema Dkt. Magufuli.
Aliendelea kwa kusema kuwa TCU
imekuwa ikiwachagulia wanafunzi vyuo visivyo na sifa na makazi ya wanafunzi
hivyo kusababisha wanafunzi hao kusoma katika mazingira magumu na wanapomaliza
masomo yao hukosa ajira kutokana na vyuo hivyo kutokuwa na sifa.
Aidha, Rais Magufuli ameuagiza
uongozi wa UDSM kutoza wanafunzi gharama ya shilingi mia tano(500) kama malipo
ya makazi ya mabweni hayo kwa siku
badala ya shilingi mia nane(800) inayotozwa kwa mabweni mengine yaliyopo chuoni
hapo.
Alisema kuwa Serikali ya Awamu ya
Tano imejipanga kuwekeza katika elimu hivyo itahakikisha wanafunzi nchini
wananufaika kwa kupata elimu bora kuanzia shule za msingi hadi vyuo vikuu.
“watanzania walinichagua ili
kutatua changamoto zinazowakabili na hivi ndivyo ninavyofanya kutatua
changamoto hizo” alisema Rais Magufuli.
Naye, Waziri wa Elimu Sayansi na
Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako amempongeza Rais Magufuli kwa kutoa shilingi
bilioni 10 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni hayo ambao kwa kiasi kikubwa yatatatua
changamoto ya makazi iliyokuwa ikiwakabili wanafunzi wa chuo hicho.
Prof. Ndalichako amesema kuwa
mabweni hayo yamejengwa kwa kipindi cha miezi 8 ambayo yatachukua wanafunzi
3840.
Kwa upande wake Makamu Mkuu wa
Chuo cha Kikuu cha Dar es Salaam Prof. Rwekaza Mukandala ametoa rai kwa
wanafunzi wa chuo hicho kuhakikisha wanaimarisha usalama katika maeneo ya
mabweni hayo na kulinda miundo mbinu yote iliyoweka.
“Ni lazima mzingatie matumizi
sahihi ya kila kifaa kilichofungwa katika majengo haya, majengo haya ni mapya
na yamejengwa kwa gharama kubwa kwa lengo la kutusaidia kuondokana na
changamato iliyotukabili kwa muda mrefu,” alisema Prof. Mukangala.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Profesa Rwekaza Mukandala wakati akiwasili kuzindua majengo mapya ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam eneo la Mlimani jijini Dar es salaam. Kiushoto ni Mama Janeth Magufuli na kulia ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Arch. Elius Mwakalinga. Mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3840, yamejengwa chini ya muda wa mwaka mmoja na yamegharimu shilingi bilioni 10.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongozana na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Profesa Rwekaza Mukandala wakati akiwasili kuzindua majengo mapya ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam eneo la Mlimani jijini Dar es salaam.Mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3840, yamejengwa chini ya muda wa mwaka mmoja na yamegharimu shilingi bilioni 10.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea zawadi ya mchoro toka kwa Rais wa Wanafunzi wakati wa sherehe za kuzindua majengo mapya ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam eneo la Mlimani jijini Dar es salaam. . Mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3840, yamejengwa chini ya muda wa mwaka mmoja na yamegharimu shilingi bilioni 10.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wakati wa sherehe za kuzindua majengo mapya ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam eneo la Mlimani jijini Dar es salaam. Kulia ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Arch. Elius Mwakalinga. Mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3840, yamejengwa chini ya muda wa mwaka mmoja na yamegharimu shilingi bilioni 10.
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...