Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, waandaaji wa tamasha hilo, Alex Msama (wa nne kushoto), akimkabidhi Tuzo aliyomtunuku Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Mgeni rasmi wa tamasha hilo, Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mwigulu Nchemba aliyeipokea kwa niaba yake, wakati wa tamasha hilo.  
Wachungaji walioohudhuria tamasha hilo, wakimwombea mwimbaji, Solly Mahlangu (chini aliyepiga magoti), kutoka Afrika Kusini, wakati alipotumbuiza kwenye tamasha hilo jana jijini. 
Mwimbaji wa nyimbo za Injili, Martha Mwaipaja, akitumbuiza katika tamasha hilo.  
Mashabiki waliohudhuria katika Tamasha la Pasaka wakifuatilia matukio mbalimbali yaliyokuwa yakitendeka na kupiga picha za selfi, uwanjani hapo. 
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, waandaaji wa tamasha hilo, Alex Msama (kulia), akiimba sambamba na mwimbaji wa nyimbo za Injili, Martha Mwaipaja, wakati akitumbuiza katika tamasha hilo. 
Mgeni rasmi wa tamasha hilo, Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mwigulu Nchemba, akipongezwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (kushoto), mara baada ya kumaliza kutoa hotuba yake. Katikati ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, waandaaji wa tamasha hilo, Alex Msama.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...